• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Malima atekeleza ahadi kwa Fire Volunteers.

Posted on: February 6th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima ametekeleza ahadi yake aliyoitoa hivi karibu kwa Vijana wanaojitolea katika Jeshi la Zimamoto (Fire volunteers) waliounga mkono zoezi la uokoaji watu na mali zao baada ya kutokea mafuriko ya Januari 24, 2024 katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Mhe. Malima amesema hayo Februari 5, 2024 wakati akikabidhi fedha taslimu kiasi cha shilingi 1,600,000/= kwa Vijana hao wa Fire Volunteers katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

Mkuu huyo wa Mkoa ameeleza kuwa mnamo Januari 24, mwaka huu yalitokea mafuriko maeneo mengi ya Mkoa huo ikiwemo maeneo ya Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro ambayo yalisababisha uharibifu wa miundombinu na mali za wananchi lakini Vikosi mbalimbali vilijitoa kusaidia zoezi la uokoaji.

Miongoni mwa vikosi hivyo ni pamoja na Fire Volunteers kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokaoji huku akibainisha kuwa alivutiwa kuona vijana hao wanajitoa kusaidia waathirika wamafuriko hayo na kuahidi kutoa milioni moja ili iwasaidie.

“...siku ile pale nikakuta kuna watu Volunteers maaskari wa Zimamoto na Uokozi wa kujitolea sasa lile jambo binafsi likanipa faraja kubwa sana...hnilisema mimi binafsi nitatoa milioni moja mkapate hata sababuni kwa wale watu 33 waliokuwepo pale...” amesema Mkuu wa Mkoa.

Aidha, Mhe. Malima amesema Ofisi ya Mkuu wa Mkoa itagharamia mafunzo ya muda mfupi ya ujuzi wa uokoaji yatakayopangwa siku za usoni ya Vijana hao huku Ofisi hiyo kwa kushirikiana na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoani humo itahamasisha wadau wengine kuchangia vifaa wakati wa mafunzo ya vijana hao.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amewaasa vijana hao kuwa na nidhamu, maadili mema, utayari na kutambua kuwa jambo hilo ni la kujitolea hususan katika kipindi chote cha mafunzo.

Naye Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Morogoro Shabani Marugujo amesema lengo la kuanzisha Fire Volunteers ni kutokana uwezekano wa kutokea kwa majanga ya moto na mafuriko yanayosababishwa na kukua kwa teknolojia, ongezeko la watu na ukuaji wa miji, hivyo amesema Vijana hao ni muhim kuwa nao ili kuongeza nguvu katika zoezi la uokoaji.

Aidha, amebainisha kuwa Mkoa wa Morogoro kwa sasa una vijana wa Fire Volunteers 74 huku akisema kuwa namba hiyo itaongezeka kutokana na mwamko wa Vijana kujiunga na kikundi hicho.

Kwa upande wake Kiongozi wa kikundi cha Fire Volunteers Mkoa wa Morogoro Salumu Selemani amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kutimiza ahadi yake na kuongeza kuwa wameamua kuanzisha kikundi hicho kwa lengo la kuisaidia jamii wakati wa majanga.

Sambamba na shukrani hizo, Bw. Salum amewataka wananchi kuendelea kuchukua taadhari dhidi ya majanga ambapo amewataka kupiga namba 114 kwa ajili ya kutoa taarifa mara wanapofikwa na majanga ya aina hiyo ili kupatiwa msaada.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.