• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA ATEMA CHECHE TABIA YA KUWANYANYASA NA KUWANYANYAPAA WAZEE.

Posted on: October 2nd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amekemea vikali tabia ya baaadhi ya watu  kuwanyanyasa na kuwanyanyapaa wazee jambo ambalo ni kinyume na sheria na taratibu za nchi ambapo amesema jambo hilo hupelekea  kudhohofisha maendeleo ya wazee.

Mhe. Malima ametoa kauli hiyo Oktoba 1, 2024 wakati akizindua bwalo la wazee wa kituo cha Fungafunga pamoja na kusheherekea na kula chakula pamoja na wazee hao katika ukumbi  wa kituo hicho kilichopo katika Halmashauri ya Manipsaa ya Morogoro.

Amesema, pindi wazee wanapotoka katika makazi yao na kupelekwa vituo vya kulelea wazee  mali zao wanazoziacha katika makazi yao zitaendelea kuwa zao, hivyo amemtaka mwakilishi wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kuliangalia suala hilo na kuweka sheria ya kuwalinda wazee kwa sababu imekuwa ni tabia ya baadhi ya watoto kuwapora mali wazee na kusababisha wazee kukosa haki zao.

".. Nikisema hili wanamorogoro wanisikie vizuri hii tabia ya kuwanyanyasa na kuwanyanyapaa wazee hiyo habari iishe kabisa kwa sababu hiyo ni akili ya watu wasiojielewa.." amesema Mhe. Adam Malima.


Aidha, Mhe. Malima amesema kituo hicho cha Fungafunga kinaweza kuhifadhi wazee 108 ambapo kwa sasa wapo wazee 23, hivyo amewataka wataalamu wa maendeleo ya Jamii kuliangalia suala hilo la  kuwatafuta wazee wenye uhitaji katika Mkoa wa Morogoro na kuwapeleka eneo hilo kwa sababu nafasi bado ipo.

Sambamba na hayo, Mkuu huyo wa Mkoa amesema suala la kuwapatia wazee huduma zao stahiki hasa huduma za Afya ni suala la lazima sio hiari, hivyo amewataka wakurugenzi wa halmashauri za Mkoa huo kuhakikisha suala la huduma kwa wazee linazingatiwa ili uhitaji wa huduma muhimu kwa wazee upapatikane kwa urahisi.

".. Hili suala la huduma kwa wazee litakuja kuwapa watu balaa tafuteni vitu vingine vya kufanyia masihara lakini sio jambo hili.." Amesisitiza kiongozi huyo.


Katika hatua nyingine Kiongozi huyo ametoa shukrani za dhati kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kujali wazee kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya wazee na kuwakumbuka mara kwa mara hususan wakati wa sherehe mbalimbali.

Mwisho, Mhe. Malima amepokea changamoto zilizotolewa na wazee hao ikiwemo changamoto ya ubovu wa barabara inayoingia katika kituo hicho jambo ambalo amesema anaenda kulifanyia kazi na kuhakikisha barabara hiyo inapitika kipindi chote cha mwaka.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.