• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Malima atembelea Ujenzi wa barabara ya Kidatu - Ifakara, atoa maagizo

Posted on: November 7th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Ali Malima ametembelea ujenzi wa barabara ya Kidatu - Ifakara inayojengwa kwa kiwango cha lami pamoja ujenzi wa Daraja la Ruaha na kuona utekelezaji wake huku akitoa maagizo kwa Mkandarasi anayejenga kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa km 66.9 ifikapo mwezi Machi, 2024.


Daraja jipya la Ruaha linaloendelea na ujenzi

Mhe. Adam Kighoma Malima ametoa maagizo hayo Novemba 7 mwaka huu wakati wa ziara yake ya siku mbili katika Wilaya za Kilombero na Ulanga na kufika eneo la mradi wa daraja hilo akiambatana na Wajumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na kutoa maagizo hayo huku ikataka viongozi wa Wilaya ya Kilombero kuendelea kushirikiana na Mkandarasi huyo ili akamilishe ujenzi huo kwa wakati.

Daraja la zamani linalotumika 

"...matarajio yangu mimi ni kwamba muda huu tuliokubaliana basi hatutarajii kuona changamoto zingine hapo katikati, hapana..." amesema Mkuu nuyo wa Mkoa.

Akimsisitizia Mkandarasi huyo amesema, changamoto zozote zikiwemo mvua na nyingine zikiwapo anatakiwa kukabiliana nazo na kuongeza kasi ya ujenzi hususan wa Daraja hilo usiku na mchana kwa kuwa mradi huo ni wa muda mrefu na wananchi wanauhitaji ili kuonja matunda ya mradi huo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akishuka katika Daraja la Ruaha baada ya kukagua Daraja hilo.

Katika hatua nyingine Mhe. Malima amesema mradi huo ni kichocheo cha maendeleo katika ukanda wa bonde la Mto Kilombero kwa vile daraja na barabara hiyo ni kiunganishi pekee baina ya Wilaya zote za Ulanga, Malinyi na Kilombero lakini pia kiunganishi baina ya Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Songea ambapo kwa kukamilika kwake changamoto usafiri wa watu na usafirishaji wa bidhaa hususan mazao itakuwa imetatuliwa lakini pia itakuwa ni rahisi kufika Mkoa wa songea kwa kupitia barabara hiyo.

Mradi mwingine uliotembelewa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Adam Malima ni kituo cha kupoozea umeme kinachojengwa Mjini Ifakara ambacho ujenzi wake umefikia 99% na unatarajiwa kukamilika Mwezi Novemba 18, 2023 kwa gharama ya Tsh bil. 19.

Miongoni mwa mitambo ya kituo cha kupoozea umeme ikiwa tayari Kwa kuanza kazi.

Miradi hii yote inayoendelea kutekelezwa ndani ya Mkoa wa Morogoro ni juhudi za Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima amemshukuru Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa pesa za miradi hiyo ya kimkakati na mingine mingi kwa ajiri ya wananchi wa Mkoa huo.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.