• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA ATOA MAAGIZO KWA VIONGOZI WA SERIKALI.

Posted on: September 29th, 2024


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewaagiza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Mkoa wa huo kuhakikisha wanafanya utambuzi wa wazee ndani ya Mkoa huo ili kuweza kufahamu idadi yao, kuwafikia na  kuhakikisha wanapata huduma bora hususan huduma za Afya.

Mhe. Adam Malima ametoa agizo hilo Septemba 21, 2024 wakati wa maadhimisho ya siku ya wazee Duniani ambayo kimkoa yamefanyika Wilayani Gairo yakiambatana na kauli mbiu inayosema "Tuimarishe huduma kwa wazee, Wazeeke kwa Heshima".

Amesema, Mkoa wa Morogoro umefanya utambuzi wa wazee 56,000 ambapo wazee 51,000 kati yao wamepatiwa msamaha wa huduma mbalimbali, hivyo bado kuna umuhimu mkubwa wa kuongeza jitihada ya kuwatambua ili kuhakikisha wanapata huduma zilizo bora na kwamba suala la wazee kupata huduma sio la hiari bali ni la lazima kwa sababu ni haki yao ya kimsingi.

"..Ninatoa maagizo kwa wakuu wa Wilaya na kwa Wakurugenzi, muende mkafanyie kazi suala la utambuzi wa wazee ili tuweze kuwafikia na kuhakikisha kwamba wanapata haki zao.." amesisitiza Mhe. Adam Malima.

Akibainisha zaidi, Mkuu huyo wa Mkoa amesema Mkoa huo una jumla ya vikundi vya wazee wajasiliamali 25 ambapo vikundi 21 vipo Halmashauri ya Manispaa, Wilaya ya Kilosa 1, Mvomero 2, na Gairo 1 huku akiutaka uongozi wa wazee wa Morogoro kwenda kutoa elimu na kuhamasisha wazee kujiunga na vikundi vya ujasiliamali yakufanya biashara ndogondogo.

Aidha, Mhe. Malima amekemea vikali tabia ya baadhi ya vijana ya kuwapokonya wazee wao mali na kuzitumia jambo ambalo amesema ni kinyume na sheria na taratibu za nchi na kuwaagiza wazee ndani ya Mkoa huo kutofumbia macho masuala hayo na pindi matukio hayo yakitokea watoe taarifa haraka ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria.

Katika hatua nyingine Mhe. Malima ametumia fursa hiyo kuwataka wakazi wa Morogoro wenye sifa ya kupiga kura kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la kupiga kura na ifikapo Novemba 27, 2024 kwenda kupiga kura kwa sababu kuchagua na kuchaguliwa kuwa kiongozi ni haki ya kila mtanzania.

Akifafanua zaidi kiongozi huyo amebainisha kuwa  Oktoba 11 hadi 20, 2024 kutakuwa na zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura huku akiwataka wazee kujitokeza kupiga kura lakini pia kuwahamasisha vijana kujitokeza kujiandikisha na kupiga kura ili kupata viongozi bora wa kuwaletea maendeleo yao na taifa kwa jumla.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Wazee Mkoa wa Morogoro Bw. Samwel Mpeka ametaja baadhi ya changamoto zinazowakabili wazee zikiwemo za kubaguliwa ndani ya jamii kwa sababu ya imani potofu, kutelekezwa na familia zao kutokana na ugumu wa maisha.


Changamoto nyingine ni pamoja na kutopata huduma za Afya na madawa, kwa sababu hiyo kupitia maadhimisho hayo ameiomba serikali kuendelea kuboresha huduma za Afya hasa utoaji wa dawa kwa wazee na kuendelea kutoa kadi za msamaha kwa wazee.


Naye Mkurugenzi wa Shirika la Wazee Mkoa wa Morogoro (MOROPEO) Bw. Samson Msemembo amesema kukomeshwa kwa ukatili wa mauaji ya wazee vikongwe, kudharauliwa na kunyanyapaliwa na kuimarisha hali ya maisha na ustawi itasaidi  wazee wa nchi hii waishi kwa heshima.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.