• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA ATOA USHAURI WA BURE KWA MADIWANI KILOSA.

Posted on: June 25th, 2024


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewaagiza Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa kujiwekea utaratibu wa kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa kila kikao cha baraza lao ili kuiepusha uwepo wa utitiri wa hoja zinazopelekea kukwamisha maendeleo ya wananchi.

Mkuu wa Mkoa Adam Malima ametoa agizo hilo Juni 25 mwaka huu wakati wa kikao maalum cha Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo kilicho ukumbi wa FDC Ilonga Wilayani humo.

Maagizo hayo yamekuja baada ya Halmashauri hiyo kuwa na jumla ya hoja 27 zilizoibuliwa na CAG za tangu mwaka 2016/20217 na kupelekea kutotekelezwa kwa miradi ya maendeleo yenye jumla ya zaidi ya shilingi 1.8 Bil.

“nakuombeni sana ninyi madiwani, kila kikao chenu cha Baraza la madiwani muwe na ajenda za hoja za CAG” amesema Mhe. Malima.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewataka waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri hiyo ya kilosa Kwenda kusimamia vema maendeleo ya wananchi wao ili wapate sifa zitakazowawezesha uchaguzi wa mwakani kurudi  kwenye nafasi zao.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoamwa Morogoro amewataka watendaji wote wa Mkoa huo kufanya kazi kwa mujibu wa sheria, Taratibu na Kanuni zilizowekwa na kutoa onyo kwa watendaji watakaokwenda kinyume na miongozo hiyo watachukuliwa hatua za kinidhamu.

Aidha, amewataka Wahe. Madiwani pamoja na kuwa Serikali inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan inatoa fedha nyingi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi, bado amewataka Madiwani kuwa wabunifu katika kuanzisha miradi ya maendeleo ikiwa ni alama ya nje ya kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Akitoa ushauri kwa madiwani na watendaji wa Serikali, Mkaguzi Mkuu wa Nje Mkoa wa Morogoro Bw. Baraka Mfugale amewataka kutoa ushirikiano wa kutosha wanapoomba nyaraka mbalimbali wakati wakitafuta majibu ya kufunga hoja, ili hoja hizo ziweze kufungwa mapema kabla hazijaingia kwenye vikao kama vinavyofanyika sasa.

Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ilibaki na hoja za miaka ya nyuma 2016/2017 hadi 2021/2022 ikiwa na jumla ya hoja 27 na mwaka wa fedha 2022/2023 jumla ya hoja mpya 12 ziliibuliwa.


Katika kutekeleza hoja hizo zilizoibuliwa na CAG, hoja 25 za nyuma kati ya hoja 27 zimekwishafungwa na kusaliwa na hoja mbili sawa na 92.59%. Aidha, hoja mpya 7 kati ya 12 zimefungwa na kusaliwa na hoja 5 sawa na 82%.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.