• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA ATOA WITO KWA WANANCHI KUSHIRIKI MAADHIMISHO MIAKA 80 YA HOSPITALI, AMSHUKURU RAIS SAMIA.

Posted on: May 13th, 2025



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewataka wakazi wa Mkoa huo na maeneo jirani kujitokeza kwa wingi kushiriki maadhimisho ya miaka 80 ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro tangu kuanzishwa kwake na kuwataka wakazi hao kushiriki matembezi ya hisani kwa ajili ya maboresho ya Hospitali hiyo.

Ametoa wito huo Mei 13, 2025 wakati anaongea na waandishi wa habari  kuelezea tukio la  maadhimisho ya miaka 80 ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Morogoro yatakayofanyika Mei 17, 2025 yakiwa na kaulimbiu inayosema "MIAKA 80 YA UJENZI WA JAMII YENYE AFYA ".

Mhe. Malima amesema, lengo la maadhimisho hayo ni kuakisi huduma za Afya za hospitali hiyo  zilizoanza kutolewa tangu mwaka 1945 na kuonesha maendeleo makubwa kwa miaka hiyo 80 na hivyo kuona umuhim wa kuadhimisha mafanikio ya Hospitali hiyo kwa kufanya matembezi ya hisani ili kuboresha baadhi ya miundombinu ya Hospitali hiyo.

"...nitumie fursa hii kutoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Morogoro kushiriki kikamilifu katika maadhimishohayo na matembezi ya hisani." Amesisitiza Mhe. Adam Malima


Aidha, kiongozi huyo amesema maadhimisho hayo yalianza na programu ya upimaji wa Afya kwa wananchi tangu Mei 5 hadi Mei 9 mwaka huu ambapo jumla ya wananchi 3,772 wamepatiwa huduma za vipimo  (Afya Check)  na kufanyiwa huduma za upasuaji  wagonjwa 170 bure hususan wagonjwa walioshindwa kupata huduma hizo kwa sababu za kukosa fedha na kwamba huduma za upasuaji zinaendelea kutolewa hadi tarehe 16 Mei, 2025 ili kukamilisha upasuaji kwa wagonjwa 242 waliokusudiwa.

Katika hatua nyingine Mhe. Malima amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kutoa fedha nyingi kwa kipindi kifupi cha miaka yake minne ya uongozi Wake katika sekta ya Afya ambapo Hospitali hiyo imepokea zaidi ya shilingi billioni 7.8 kwa ajili ya kuboresha hudumaza Afya Pamoja na kuboresha miundombinu ya kutolea huduma za dharura.


Amebainisha pia kuwa fedha hizo zimesaidia kujenga majengo ya huduma za dharura, jengo la wagonjwa mahututi, uwekaji vifaa vya kisasa vya kutolea huduma kama CT Scan, Digital X-Ray, Mtambo wa kufua hewa tiba ya oksjeni, Kifaa cha uchunguzi wa sikio, koo, pua, mashine kumi za kuchuja damu (Dialysis) na uboreshaji wa huduma za Daraja la kwanza.


Hospitali  ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro  inatimiza miaka 80 tangu ilipoazishwa mwaka 1945 ikiwa kama kituo cha kutolea huduma za Afya kwa majeruhi wa vita ya pili ya Dunia iliyoanza mwaka 1939 - 1945.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI SHERIA, KATIBA NA KANUNI YA VYAMA VYENU - MUTUNGI.

    May 14, 2025
  • WANAFUNZI 214 WA KIDATO CHA KWANZA SEKONDARI ZA MONGOLA, MGETA WAPEWA MICHE 2140 YA MIKARAFUU

    May 13, 2025
  • RC MALIMA ATOA WITO KWA WANANCHI KUSHIRIKI MAADHIMISHO MIAKA 80 YA HOSPITALI, AMSHUKURU RAIS SAMIA.

    May 13, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.