• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AWAALIKA WANANCHI KUSHIRIKI MAONESHO YA NANENANE

Posted on: July 29th, 2025



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima, ametoa wito kwa wananchi wa mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Tanga na Morogoro kushiriki Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yatakayoanza kufanyika kuanzia Agosti 1 hadi Agosti 8, 2025.

Mhe. Malima ametoa wito huo leo Julai, 29, 2025 wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi yake na kubainisha kuwa maonesho hayo yanaenda sambamba na kaulimbiu inayosema;

“Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, 2025.”

“Nitoe wito kwa wananchi wa mikoa hii minne, hususan wenyeji wa Mkoa wa Morogoro, kufika kwa wingi katika Viwanja vya Maonesho vya Mwalimu Julius K. Nyerere na kushiriki kikamilifu katika maonesho haya,” amesisitiza Mhe. Adam Malima.

Amesema, maandalizi ya maonesho hayo yamekamilika kwa asilimia 98, huku maboresho mbalimbali yakiendelea. Moja ya maboresho hayo ni upatikanaji wa maji changamoto ambayo imekuwa sugu kwa wadau wa maonesho hayo.

Aidha, ametumia fursa hiyo kumshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na Serikali yake kwa kutoa fedha zilizotumika kuchimba visima vya maji na kusambaza kwa wananchi na eneo la Viwanja vya Maonesho ya Nanenane.

Mhe. Malima amewataka viongozi wa Serikali mkoani humo kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wananchi wakati wote wa maonesho hayo, huku akiwahakikishia washiriki ulinzi wa kutosha ndani ya viwanja vya nanenane kanda ya Mashariki na Mkoa mzima kwa jumla.

Katika hatua nyingine Mhe. Adam Malima amesema Maonesho ya Nanenane ya mwaka huu yatahusisha jukwaa maalum la B2B (Business to Business), litakalotumika kutoa mada zinazohusu Sekta ya Kilimo, Mifugo, Uvuvi na mazao yatokanayo na misitu zitakazowasilishwa na wakufunzi wabobezi kutoka taasisi mbalimbali za Serikali.


Amesema, mada hizo zitatolewa bila malipo kuanzia Agosti 2 hadi hadi Agosti 7 na kwa sababu hiyo amewataka wananchi wote wenye nafasi kushiriki jukwaa hilo ili kupata maarifa na ujunzi katika masuala ya kilimo, Mifugo, Uvuvi na masuala na misitu.


Mgeni rasmi wa maonesho hayo ya Nanenane kanda ya Mashariki mwaka 2025 yanayotarajiwa kuanza Agosti 1 na kufunguliwa rasmi Agosti 2 ni Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Baraza la taifa la Uashauri wa Rais wa masuala ya Kilimo.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Mhe. Rais afanyiwa tambiko na wazee wa kimila Morogoro

    August 28, 2025
  • RC Malima atoa siku saba kuunda SACCOS

    August 22, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA VIJANA KUTATUA CHANGAMOTO ZAO

    August 12, 2025
  • WADAU WA MAONESHO YA NANENANE WAAGIZWA KUTEKELEZA WALIYOJIFUNZA

    July 12, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.