• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AWATAKA MADIWANI KUSIMAMIA MAENDELEO

Posted on: June 29th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewataka  wahe. Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kusimamia miradi ya maendeleo kikamilifu  kwa kuwa Halmashauri hiyo ni moja ya majukumu yao ya Msingi  katika kuhakikisha wanawapelekea wananchi maendeleo na kukuza kipato chao.

Mhe. Malima ametoa agizo hilo Juni 29, 2024 wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani cha kujadili hoja za Mdhibiti na  Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya hiyo Mkoani Morogoro.

Kiongozi huyo amesema, kuna umuhimu mkubwa kwa wahe. Madiwani wa Halmashauri hiyo kusimamia miradi ya maendeleo inayopelekwa na Serikali kwa wananchi, hivyo wanatakiwa kuwajibika katika kuisimamia miradi hiyo na endapo watashindwa kuisimamia watakuwa wameshindwa kufanya kazi yao ya msingi.

“.. Kazi yenu madiwani ni kusimamia miradi ya maendeleo, madiwwni wasiosimamia ni sawa na mtu anayeulizwa swali kuhusu kwake halafu hajui…” amesema Adam Malima.

Kiongozi huyo amebainisha ndani ya kikao hicho, kazi nyingine za msingi za Wahe. Madiwani ukiachia usimamizi wa miradi ya maendeleo ni pamoja na kusimamia matumizi ya fedha za Serikali na kusimamia Halmashauri zao katika ukusanyaji wa mapato ya ndani ya halmashauri zao.

Katika hatua nyingine, Mhe. Malima ameagiza watumishi wa Halmashauri hiyo ambao hawajahamia makao Makuu ya Halmashauri hiyo, kuhamia mara moja kabla au ifikapo Agosti 1, mwaka huu na ambaye hatatekeleza agizo hilo hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yake.

Aidha, ameelekeza kuwa watendaji wote ambao wanakabiliwa na tuhuma za ubadhilifu wa fedha au mali za Umma ambao wametajwa kwenye Hoja za CAG, watumishi hao watafutwe na jeshi la polisi, wakamatwe na wafikishwe kwenye vyombo vya sheria ama mamlaka zinazohusika.

Akisisitiza katika mfumo wa stakabadhi  ghalani, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka Wahe. Madiwani kutumia mfumo huo katika kuuza mazao ya wakulima wa Halmashauri hiyo kwa kuwa unamlinda mkulima kutonyonywa na una maslahi mapana kwa Halmashauri yao.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amewataka watendaji wa halmashauri hiyo kufanya kazi zao kwa kufuata Sheria, Taratibu na Kanuni zilizopo, akisisitiza masuala mengi ikiwemo utunzaji wa siri za Ofisi, kutojihusisha na rushwa, usimamizi madhubuti wa miradi ya maendeleo na uwasilishaji wa fedha Benki za makusanyo ya ndani ya halmashauri.

Kwa upande mwingine amewashauri Wahe. Madiwani pamoja na kutekeleza miradi iliyoletwa na Serikali na kutekeleza kilimo cha mazao ya  kimkakati kikiwemo kilimo cha zao la michikichiki, parachichi, Kokoa, Chai na mazao ya viungo kama Karafuu bado kuna fursa nyingi za kuzitumia katika kukuza uchumi wa wananchi wao ikiwemo matumizi sahihi ya mashina ya migomba ambayo huzalisha nyuzi za kutengenezea vifaa mbalimbali vinavyotumika na jamii.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Lucas Lemomo wakati akiahirisha kikao hicho kwa niaba ya Wahe. Madiwani  wengine ametumia fursa hiyo kupongeza  uongozi wa Mkoa namna ulivyosaidia kuongeza nguvu katika kusimamia ujenzi wa shule za sekondari ikiwemo shule ya Mkoa wa Morogoro na pia amewataka watendaji wa Halmashauri hiyo kutekeleza maelekezo yote ya ufungaji wa hoja za CAG kama kikao hicho kilivyoelekeza.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.