• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AWATAKA WANANCHI KUFANYA MAPINDUZI YA KILIMO MOROGORO.

Posted on: October 12th, 2024



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewataka wananchi wa Wilaya ya Gairo na Mkoa kwa ujumla kufanya mapinduzi ya Sekta ya Kilimo hususan Kilimo biashara kutekeleza kwa vitendo ili kuongeza thamani katika Sekta hiyo na kuwa mfano kwa Watanzania wote.


Mhe. Malima amesema hayo Oktoba 12, 2024 wakati akifunga maonesho ya SAMIA KILIMO BIASHARA EXPO 2024, MSIMU WA 3 yaliyofanyika Wilayani Gairo kuanzia Oktoba 6 - 12, Mwaka huu yakiwa na lengo la kuwasaidia wakulima na wafugaji kupata huduma na kujifunza teknolojia mpya na mbinu bora za uzalishaji.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesema maonesho hayo yamefanyika kwa msimu wa tatu katika Halmashauri ya Wilaya ya Gairo hivyo amewataka wananchi hao kuchangamkia fursa katika sekta ya Kilimo kama wanavyo himizwa ili kuleta mapinduzi makubwa ya kilimo, kuongeza mapato,  kuboresha maisha na kujipatia kipato kwa uzalishaji wa wenye maslahi mapana ya nchi.

"..Ombi langu mimi hii jitihada kubwa inayofanywa ili wananchi wa Gairo wanufaike na mapinduzi ya Kilimo nakuombeni msiwe watu wa kusikiliza bila kufanyia kazi, muwe mnayafanyia kazi na watanzania wengi watakuja kuiga kutoka kwenu.." Amesisitiza Mhe. Adam Malima.

Pia Mhe. Malima amewataka wananchi wa Wilaya hiyo kulima mazao ya kimkakati  yakiwemo Tumbaku, mbaazi, parachichi ili kuondokana na umasikini kwani kilimo Wilayani humo ni muhimili wa vipato vya wananchi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Malima amewaagiza wataalamu wa kilimo kuendelea kushirikiana na wakulima na wafugaji ili kupata uelewa kuhusu matumizi ya pembejeo za kilimo, mbegu, mbolea na sumu za kuua wadudu kwa uzalishaji wenye tija na kuongeza mapato katika Halmashauri hiyo na Taifa kwa ujumla.

Mhe. Adam amehimiza wananchi wa Wilaya hiyo kutumia nishati safi ya kupikia ikiwa ni kuunga mkono ajenda ya Mhe. Dkt. Samiaa Suluhu Hassan kwa maono ya kutumia nishati safi ya kupikia ikiwemo Gesi, umeme, mkaa mweupe na nyingine ili kuepuka magonjwa yasiyo ya kuambukizwa yakiwemo magonjwa ya kansa ya mapafu, uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabia nchi.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Dkt. Rozalia Rwegasira akiongea kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa huo Dkt. Mussa Ali Mussa amesema zaidi ya asilimia 65% ya wananchi wa Mkoa huo wanategemea kilimo hivyo amewataka wananchi hao kufanya kilimo chenye tija.


Kwa sababu hiyo, Kiongozi huyo ametoa wito kwa viongozi mbali mbalimbali wakiwemo Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Tarafa, Katibu Tawala wa Wilaya, Watendaji wa Kata, Maafisa kilimo na Maafisa Ugani waliopo ngazi ya Kata na vijiji kuhakikisha elimu za kilimo bora zinawafikia wananchi.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.