• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MALIMA AZINDUA UJENZI WA STENDI ITAKAYOTUMIKA KUHUDUMIA ABIRIA WANAOSAFIRI NA RELI MWENDOKASI

Posted on: July 24th, 2025


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, amezindua rasmi ujenzi wa stendi ya mabasi ambayo itaunganishwa na Kituo cha Reli ya Mwendokasi cha Jakaya Mrisho Kikwete cha mjini Morogoro, ujenzi utakaogharimu zaidi ya shilingi bilioni 13.4 Mradi unatarajiwa kukamilika Julai 21, 2026.


Mhe. Malima amefanya uzinduzi huo Julai 23, 2025 huku akiwataka wafanyabiashara wa Mkoa huo kuchangamkia fursa hiyo kwa kuwekeza katika eneo hilo ili kulifanya liwe la kisasa na kuongeza mapato ya Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.


Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amezitaka taasisi zinazoshughulikia maji, umeme, barabara na Halmashauri yenyewe kuhakikisha huduma hizo zinapatikana kabla ya kukamilika kwa ujenzi huo ili stendi hiyo iweze kuwa bora na ya kisasa hivyo kutoa huduma za kiwango cha juu kwa wananchi.


Mhe. Malima ametumia fursa hiyo kumshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kutoa fedha hizo kwa ajili ya ujenzi wa stendi hiyo, akisema kuwa ni ishara ya dhamira yake ya dhati ya kuhakikisha wananchi wa Morogoro wanapata huduma bora na kwa wakati.


Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Morogoro, Bw. Emmanuel Mkongo, amesema ujenzi huo utahusisha majengo mbalimbali, likiwemo jengo la ghorofa moja litakalojumuisha hoteli yenye vyumba 30 vya kulala wageni, eneo la vinywaji na burudani, ukumbi mkubwa wa mikutano na ndogo nne na maduka.


 Maeneo mengine ya jengo hilo ni mabanda ya kisasa kwa ajili ya mama lishe na baba lishe, kituo cha polisi, maeneo ya kupaki mabasi, bodaboda na bajaji, pamoja na sehemu za kukaa abiria na kubainisha kuwa ujenzi huo utarahisisha huduma za usafiri na usafirishaji wa abiria kutoka kituo hicho kwenda maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya Manispaa.


Naye Ramadhani Juma Mfinanga mwananchi wa Manispaa ya Morogoro ambaye pia ni dereva wa bajaji, ameishukuru Serikali inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kujenga mradi huo, kwani amesema utaongeza idadi ya abiria, jambo litakalowaongezea kipato na kuboresha maisha yao.


Mwisho






Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Mhe. Rais afanyiwa tambiko na wazee wa kimila Morogoro

    August 28, 2025
  • RC Malima atoa siku saba kuunda SACCOS

    August 22, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA VIJANA KUTATUA CHANGAMOTO ZAO

    August 12, 2025
  • WADAU WA MAONESHO YA NANENANE WAAGIZWA KUTEKELEZA WALIYOJIFUNZA

    July 12, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.