• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Morogoro aagiza kukamatwa kwa Mwenyekiti

Posted on: September 2nd, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela ameliagiza jeshi la Polisi Mkoani humo kumkamata mwenyekiti wa Kijiji cha wami luhindo Wilayani Mvomero, Juma Makumlo  kwa tuhuma za ubadhilifu wa fedha za wananchi wa kijiji hicho.

Mkuu wa Mkoa huyo ametoa agizo hilo Septemba 2 mwaka huu akiwa katika ziara yake ya kikazi Wilayani Mvomero wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha Wami Luhindo.

Shigela amemtaka Mwenyekiti huyo anayetuhumiwa kukamatwa mara moja na kurejesha fedha zote alizokuwa anazipata kutoka kwa wananchi wake kwa kuwachangisha michango isiyo halali na kisha kutokomea na fedha hizo kusikojulikana.

“Nataka leo mtafute mwenyekiti, mkamate na kesho aitoe hiyo laki moja irudi kwenye kijiji” ameagiza Martine Shigela.

Kutokana na kadhia hiyo, Martine Shigela ameuagiza uongozi wa Wilaya ya Mvomero kufuata utaratibu wote wa kiutumishi na kukasimisha shughuli za mwenyekiti wa kijiji hicho kwa Mwl. David Langa ambaye atafanya kazi za kupokea michango kutoka kwa wananchi na kusimamia shughuli nyingine za kijiji hicho.

Aidha, Shigela ameuagiza uongozi huo kumsainisha mkataba Mwl. David Langa kabla ya kuanza majukumu hayo mapya huku akiwaagiza pia kuanza kumlipa mshahara wake kwa muda wote atakaokuwa anakaimu nafasi hiyo.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wananchi wa Kijiji hicho kutokuwa na hofu yoyote kila mara viongozi wa Serikali wanapopanga kutembelea Kijijini kwao kwani hawana nia mbaya badala yake wana lengo la kutaka kuwaletea kutatua nkero zao na kuwaletea maendeleo yao

 “msitishike, mimi nimekuja kutatua kero na matatizo ya wanakijiji, kama walikuwepo viongozi wenu wa vijiji wakawajengea hofu mimi nimekuja kwa ajili ya wananchi” amesema martine shigela.

Naye Mkuu wa wilaya ya Mvomero Halima Okash amesema amepokea maagizo ya Mkuu wa Mkoa aliyoyatoa na amemhakikishia kuyatekeleza na kufuatilia kwa karibu agizo la kutiwa  nguvuni Mwenyekiti anayetuhumiwa kukimbia na fedha za wananchi.

Kwa upande wao Wananchi wa kijiji cha Wami Luhindo  wamemueleza Mkuu wa Mkoa matatizo yao, akiwemo Bw. Marick Abdallah ambaye amesema mojawapo ya matatizo ya kijiji hicho ni suala zima la ujenzi wa madarasa kusimama tangu mwaka 2014, pamoja na uhaba wa madawati unaopelekea watoto wao kukaa chini.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa Martine Shigela amekagua miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani Mvomero ikiwemo bwawa la umwagiliaji  mtwiba sugar, ujenzi wa shule ya sekondari ya kumbukumbu ya hayati Moringe Sokoine pamoja na kufanya mkutano wa hadhara katika kijiji cha Manyinga kilichopo katika tarafa ya Turiani.

 

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.