• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO AAHIDI KUFANYA MASHINDANO MAKUBWA YA KUSOMA QUR - AN MWAKANI MKOANI MOROGORO.

Posted on: April 16th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa ameahidi kufanya mashindano makubwa Mkoani Morogoro ili kuendeleza vipaji vya watoto na vijana kwani madrasa huongeza maarifa,utii, juhudi, heshima na maadili mema ya kufanya vizuri kwenye masomo ya madrasa na  shuleni pia.


Amesema hayo Machi 16 Mwaka huu wakati wa Mashindano ya Qur-an yaliyoandaliwa na Umoja wa Waalim wa Madrasa wa Morogoro (UWAMAMO) yaliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Bomaroad uliopo Manispaa ya Morogoro.

Mhe. Mwassa ametatua changamoto ya vifaa kama printer itakayotumika kwa ajili ya kuchapa nakala mbalimbali ikiwemo mitihani.

“ kama nitakuwepo Mkoa wa Morogoro mwakani mwezi kama huu wa Ramadhani natarajia nishirikiane na Kamati hii kuafanya mashindano makubwa hapa Mkoani Morogoro”…. Amesema Mhe. Fatma Mwassa

Aidha, Mhe. Mwassa amewaomba wanamorogoro kuhudhuria Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mei Mosi yatakayofanyika kitaifa Mkoani Morogoro ambapo Mgeni rasmi atakuwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa UWAMAMO Alhaji Sheikh Mohamed Salim Masenga amesema lengo la Mashindano hayo ni kuhifadhi Qur-an kwa watoto na vijana ili kuepuka tabia zisizofaa kwani madrasa hufundisha vijana kuwa na nidhamu, hekima, na busara katika kupambanua mambo ya kidunia na kuilinda Qur-an isipotee.

Nae Katibu wa UWAMAMO Bw. Haafidhi Hussen Mbanachi amesema Mashindano hayo huinua uwezo na ufahamu kwa watoto na vijana katika maisha ya dini ya kiislamu na  ametoa wito kwa wazazi kufuatilia mienendo ya watoto wao watokapo madrasa.

Mjumbe na Mlezi wa UWAMAMO Bw. Bachoo Sidik Bachoo amesema mashindano hayo huondoa mabaya yaliyopo katika jamii kwani Qur-an huongoza kwa misingi na taratibu zilizopo na ni sehemu ya kulinda vijana kuingia katika mambo yasiyofaa kama ulevi, rushwa, madawa ya kulevya, na ushoga ili kuwa na idadi kamili ya nguvu kazi hapa nchini.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.