• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO AAHIDI KUTUMIA JESHI LA AKIBA KULINDA MAZINGIRA

Posted on: November 4th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa amesema atatumia Askari wa Jeshi la Akiba (Mgambo) waliopo Mkoani humo kusaidia kulinda vyanzo vya maji, hifadhi za misitu na mazingira kwa ujumla ili kuhakikisha Morogoro ya zamani inarudi katika hali yake ya awali.

Mhe. Fatma Mwassa ametoa kauli hiyo Novemba 4, mwaka huu wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya jeshi hilo la akiba kundi la 22/22 katika viwanja vya Fulwe, Tarafa ya Mikese  Wilaya ya Morogoro.

Amesema kwa mujibu wa sheria ya jeshi la akiba yeye ndiye kamanda wa jeshi hilo kimkoa, hivyo niwakati  mwafaka mwake kutumia jeshi hilo kulinda vyanzo vya maji ili kupunguza makali ya mgao wa maji na kupata umeme wa uhakika hususan umeme unaotokana na maji.

“...lakini leo nimekuja kuwaambia kwamba nyie kwa sasa sio akiba, nawahitaji sasa sio badae... nikiwa kamanda wa jeshi la akiba naanza kutumia vikosi vyangu vya jeshi la akiba...” amesema Mhe. Fatma Mwassa.

Aidha, amesema kwa sasa  Serikali ina kazi ya kulinda vyanzo vya maji, Ina kazi ya kuzuia uchomaji wa moto milimani pamoja na kulinda mipaka ya hifadhi za milima ili kuzuia wavamizi wanaojenga makazi yao katika maeneo hayo.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa ameongeza siku Saba kwa jeshi hilo la akiba kuendelea kujifunza mbinu za kuzima na kuzuia moto matukio ambayo yamekuwa sugu Katika Mkoa huo.

Hata hivyo ameagiza Mshauri wa jeshi hilo la akiba Mkoa wa Morogoro kuanzia mwakani jeshi hilo lianze kupewa  masomo ya ujasiliamali kwa kipindi chote Cha mafunzo yao ili kuwasaidia kujikwamua kiuchumi Mara wanapohitimu mufunzo yao.

Sambamba na agizo Hilo amemtaka Mshauri huyo kuratibu mafunzo ya mgambo Kufanyika Tarafa zenye vyanzo vya maji ili kuongeza ulinzi wa maeneo hayo ambayo ni muhim kwa Mkoa na taifa kwa jumla.

Akitoa tathmini ya idadi ya wahitimu wa mafunzo hayo kwa mwaka huu, Mshauri wa Jeshi la akiba Mkoa wa Morogoro Kanali Valentine Makyao amesema Wilaya ya Morogoro ndiyo imeongoza kuwa na idadi kubwa ya wahitimu wa mafunzo hayo kwa Mkoa huo kwa kuwa na wahitinu 160, ukilinganisha na Wilaya nyingine za mkoa huo.

Aidha, Kanali Makyao amesema uwepo wa jeshi hilo la akiba linaongeza uwezo wa kuimarisha Ulinzi na Usalama Katika maeneo mbalimbali hapa nchini huku akitumia fursa hiyo  kumuomba mgeni rasmi kusaidia vijana hao kupata mashamba ili wajiajiri kupitia kilimo kwa kuwa Mkoa huo ni mkoa wa Kilimo hivyo wakiwezeshwa kupitia fedha za asilimia 10, zinazotolewa na Halmashauri wanaweza kujikita kwenye Kilimo cha mazao ya kimkakati kama vile mazao ya karafuu na mkonge.

Kwaniaba ya wahitimu wa mafunzo hayo Bw. Nassoro Ally, akisoma risala mbele ya mgeni rasmi wahitimu hao wamemuomba mgeni rasmi kupewa kipaumbele kwenye ajira pindi zinapotokea  hususan zile zinazohusiana na mafunzo waliyoyapata ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuondokana na changamoto sugu ya ajira.

Mafunzo hayo ya mgambo ambayo yalianza Julai 4 mwaka huu yakiwa na wanafunzi 174, kati yao 14 hawakuweza kuhitimu kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo utoro, utovu wa nidhamu na kuugua.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.