• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO AANZA KAZI RASMI, ATOA MAAGIZO.

Posted on: May 25th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (mwenye kofia nyeupe) akisalimiana na watumishi mbalimbali wa serikali mara baada ya kuwasili katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Gairo kwa ajili ya kikao cha utambulisho. 

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima Mei 24, 2023 ameanza kazi ya kuwatumikia wananchi wa Morogoro kwa kufanya ziara ya kujitambulisha Wilaya za Gairo, Kilosa na Mvomero.

Akiwa Wilayani Gairo, Mhe. Adam Malima pamoja na maagizo mengine ameiagiza Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Wilayani humo (GAUWASA) kwa kushirikiana na Bodi ya maji bonde la Wami – Ruvu pamoja na Wakala wa maji safi na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) kuhakikisha kuwa hadi kufikia Juni 30 mwaka huu mradi wa uchimbaji visima vinne vya maji baridi uliopo eneo la Kiswiti unakamilika na wananchi wanapata huduma hiyo ya maji.

Mhe. Adam Malima (katikati) akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo  kwenye kikao cha utambulisho Wilayani humo, viongozi wengine ni Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa, Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Makame, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Gairo pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo.

“...hakikisheni kwamba tunapofika tarehe 30 mwezi wa sita kutoka kwenye chanzo hicho na milioni mia mbili hizo, watu wa Gairo wapate maji japo hicho kiducho walicha ahidiwa, pesa za mama Samia zimekuja wapate hayo maji...” amesema Mhe. Adama Malima.

Amesema hakuna sababu yoyote ya kuwacheleweshea maji wananchi wa Gairo wakati Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameshatoa fedha zaidi ya Tsh. Mil.200 kwa kwa ajiri ya Kukamilisha mradi huo.

Akiwa Wilayani Mvomero amewataka watendaji wote wa Wilaya hiyo Kila mmoja kwa nafasi yake kufuta sura mbaya iliyopo Wilayani humo ya migogoro baina ya wakulima na wafugaji badala yake kujenga sura nzuri ya Wilaya kwa kuwa Wilaya hiyo ina mazuri mengi na fursa nyingi za uwekezaji kinachotakiwa ni kwa Kila Mtendaji kufanya kazi kwa weledi na kutoa Elimu kwa makundi hayo mawili.

Aidha, amewaagiza wakala wa huduma za misitu Tanzania TFS Wilayani humo kuja na mkakati mahsusi wa kupanda miti ya kutosha.

Akiwa Wilayani Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka Mkuu wa Wilaya hiyo amempongeza Mkuu wa Mkoa Mhe. Adam Kighoma Malima kwa kuaminiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuendelea kumwakilisha kutumikia nafasi ya Ukuu wa Mkoa Mkoani Morogoro.

Aidha, Mhe. Shaka amemshukuru Rais Samia kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo katika Wilaya hiyo.

Ziara hiyo ya Mkuu wa Mkoa inaendelea kwa Wilaya zote Saba za Mkoa huo ambapo Mei 25 atafanya ziara Wilaya za Kilombero na Ulanga.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.