• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO ACHARUKA KULIPISHA WAKULIMA USHURU WA MAZAO ZAIDI YA MARA MBILI

Posted on: May 6th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela ameonekana kusikitishwa na kitendo cha baadhi ya watendaji wa Serikali kuendelea kutoza ushuru wa mazao wakulima zaidi ya mara mbili jambo ambalo amesema ni kinyume na taratibu hivyo kuwaagiza Wakurugenzi watendaji wa Halmashauri kuwataka watendaji wanaohusika na kusimamia makusanyo kuzigatia maagiz0 ya Serikali.




Martine Shigela ametoa maagizo hayo Mei 5 mwaka huu wakati akifungua kikao cha pili cha Baraza la Bisahara ngazi ya Mkoa kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Edema iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.


Amesema, bado kuna watendaji wanaotoza wakulima zaidi ya mara mbili ushuru wa mazao yao ya nafaka wanaposafirisha kutoka sehemu moja kwenda nyingine na wengine kutoza ushuru kwenye mazao ambayo hayafikii tani moja jambo ambalo amesema ni kukiuka taratibu zilizopo.



 “..kumeendelea kuwa na changamoto kwa baadhi ya halmashauri zetu, kuwa na tozo mara mbili hasa kwa mazao, mtu anatoa mpunga wake mlimba akifika Ifakara Mji anatozwa ushuru,anatoka Ifakara akifika Kilosa anatozwa ushuru…niwasihi watendaji wetu hasa wakurugenzi wa halmashauri kuwataka watendaji wetu wanaosimamia makusanyo wazingatie taratibu sheria ambazo zilishakwisha elezwa, serikali ya awamu ya sita imeendeleza kuweka misingi mizuri iliyowekwa na serikali ya awamu ya tano..” amesema Shigela

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa katika kikao hicho cha Baraza la Biashara amepongeza ushirikiano uliopo baina ya Ofisi yake na Sekta Binafsi hususan katika kuendelea kushirikiana na kutatua changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza kwa muda mrefu baina ya pande hizo mbili.



Aidha, Martine Shigela ameshauri pande hizo mbili ziendelee kudumisha mahusiano hayo, kujipanga vema na kuhakikisha wanatumia kikamilifu jitihada zinazofanywa na Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania za Kuifungua Tanzania hususan katika suala nzima la Uwekezaji.




Akiongelea eneo la uwekezaji la Star City lenye ukubwa wa ekari 6,000, Shigela amesema wameendelea kutatua changamoto za muda mrefu zilizokuwepo juu ya eneo la stsr city  lililopo Nanenane Manispaa ya Morogoro ambalo lilikuwa limekwama na kwamba tayari eneo hilo limepimwa na kuanzia sasa viwanja vimeanza kuuzwa na kutumia fursa hiyo kuwakaribisha wanaohitaji maeneo kwa ajili ya uwekezaji.




Naye mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Morogoro Mwadhini Myanza pamoja na kupongeza ushirikiano uliopo baina ya Serikali na sekta binafsi amesema bado kuna changamoto ambazo zinatakiwa kufanyiwa kazi zikiwemo changamo za kodi nyingi kuingiliana na utekelezaji wa kanuni za Service levy.



Akichangia suala la service levy Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando amewashauri Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Morogoro kuwa makini katika kuchukua ushuru huo wa service levy ili wasichukue mara mbili kwa kutojua kutokana na mwingiliano wake badala yake wakae chini na kuainisha vema ili kuwafanya wahusika kulipa ushuru huo mara moja na hivyo kudumisha mahusiano baina ya pande hizo mbili lakini pia kwa kufanya hivyo wataongeza mapato hayo mara mbili.


MWISHO

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.