• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO AKUTANA NA WADAU WA MAENDELEO KUJADILI MUELEKEO WA MKOA.

Posted on: June 2nd, 2023

Mkuu waMkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amefanya kikao na Viongozi mbalimbali wakiwemo wa  Serikali, chama, Wakuu wa taasisi za umma na binafsi na wafanyabiashara kwa lengo la kujadiliana njia sahihi ya kuyafikia mafanikio tarajiwa ya Mkoa huo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (kulia) akiteta jambo na Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro.

Kikao hicho kimefanyika Juni 1 mwaka huu kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro ambapo wadau mbalimbali wa maendeleo wamehudhuria.

Mhe. Malima amesema lengo la kukutana na wadau hao ni kujadiliana kwa pamoja ili kuwa na muelekeo mmoja wa kuyafikia mafanikio ya Mkoa huo.

"...tuzungumze na wadau wote tufahamiane na tuelewane katika hili tunalotaka kulifanya na nini tunatarajia kufanya kwa ajili ya mafanikio mapana ya Mko wetu..." amesema Mkuu wa Mkoa.

Baadhi ya Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Morogoro wakiwa kwenye kikao cha kujadili muelekeo wa Mkoa huo.

Mkuu huyo wa Mkoa amezisisitiza taasisi za umma Mkoani humo kuwa na mahusiano mazuri ili kufanikisha utendaji kazi wa taasisi hizo, akitolea mfano Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inatakiwa kuwa na mahusiano mazuri na wafanyabiashara kwa kuwa ndio wanao changia pato la Mkoa kupitia ushuru na kodi wanazozitoa.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (aliyevaa kofia) akisalimiana na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Tehama Mkoa wa Morogoro Bw. Aloyce Mbena baada ya kikao cha kujadili muelekeo wa Mkoa huo.

Nao wao wakuu wa taasisi mbalimbali walipata nafasi ya kuchangia hoja kwenye kikao hicho akiwemo Mtendaji Mkuu wa Chemba ya kilimo, biashara na viwanda Tanzania (TCCIA)Bw. Moumin Mwatawala amesema Serikali kupitia Wakala wa barabara za mijini na vijijini (TARURA) pamoja na (TANROADs) kurekebisha barabara zilizopo kwenye maeneo yanayo kusanya wafanyabiashara mbalimbali kama vile maeneo ya sokoni, standi na viwandani kurahisisha usafirishaji wa bidhaa na malighafi.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kusirye Ukio akielezea hali ya huduma za afya zinazotolewa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.

Kwa upande wake Meneja wa sheria na utawala kiwanda cha nguo cha 21st Century Bw. Nikodemus Mwaipungu amesema uzalishaji wa kiwanda hicho umepungua kutokana na changamoto ya kukatika kwa umeme na maji hivyo ameomba mamlaka husika kulifanyia kazi suala hilo ili kuongeza uzalishaji.

Baadhi ya washiriki wakiwa kwenye kikao cha kujadili muelekeo wa Mkoa wa Morogoro.

Nae Bi. Esther Mwigude ambaye ni msimamizi wa kiwanja cha ndege Morogoro kwa niaba ya Mamlaka ya viwanja vya ndege Tanzania (TAA) ameeleza mikakati ya uanzishawaji wa kiwanda kidogo cha kuunganisha vipuli vya ndege za abiria wawili, pamoja na kufungua chuo cha mafunzo ya rubani katika kiwanja cha ndege kilichopo katika Manispaa ya Morogoro.

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Rebeca Nsemwa (wa pili kutoka kulia) akiwa pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Manispaa ya Morogoro Ndg. Fikiri Juma  wakiwa kwenye kikao.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga akichangia hoja kwenye kikao cha majadiliano ya muelekeo wa Mkoa wa Morogoro.

MWISHO.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.