• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Morogoro aliagiza jeshi la Polisi kuwakamata waliohusika na ukatili kwa mtoto.

Posted on: August 31st, 2023

Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Morogoro ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Adam Malima ameliagiza jeshi la Polisi Mkoani humo kuwakamata mara moja washukiwa wa na tukio la mtoto Yohana Lyanga (3) kuchomwa na maji ya mtoto sehemu ya makalio ambaye kwa sasa amelazwa katika kituo cha Afya cha Mtakatifu Joseph Wilayani Kilosa.

Mkuu wa Mkoa Adam Malima ametoa agizo hilo Agosti 30 mwaka huu wakati wa mahojiano na waandishi wa habari akiwa katika ziara ya kutembelea kiwanda kipya cha sukari cha Mkulazi na kukutana na Kadhia hiyo ambayo ameiita ni ukatili mkubwa na usiovumilika.

Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka amesema mtoto Yohana Lyanga amefikishwa Kituo cha Afya cha Mt. Joseph Wilayani humo Agosti 29 mwaka huu akiwa na majeraha maeneo ya makalio yaliyotokana na kuchomwa na maji ya moto.

Kwa sababu hiyo, Mkuu wa MKoa huyo amekemea vikali vitendo vya ukatili wa kijinsia na watoto vinavyotokea Mkoani humo na kwamba Serikali ngazi ya Mkoa haitasita kuwachukulia hatua za kisheria wale wote wanaojihusisha au watakaojihusisha na vitendo hivyo.

“... ukatili kwa watoto hauna uhalali wa aina yoyote ile uwezi kuuhalalisha...ukatili kwa watoto, unyanyasaji wa wanawake, dhuruma dhidi ya watu masikini na vitu vyote vya ovyo ovyo vinavyo ondoa baraka katika Mkoa wetu lazima tuvipige vita...” amesema Mkuu wa Mkoa.

Sambamba na hayo, Mkuu huyo wa Mkoa amesema, hivi karibuni vitendo vya ukatili wa kijinsia hususan kwa Watoto kulawitiwa, kubakwa na kupigwa vimeongezeka katika Mkoa huo, hivyo amelaani vikali vitendo hivyo na kwamba Serikali itachukua sheria kali dhidi ya wote wanaojihusisha na vitendo hivyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka amesema Serikali inalaani vikali vitendo vyote vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na kwamba vitendo hivyo ni kinyume na sheria za nchi ya Tanzania lakini pia ni vitendo vinavyoonesha kukosa ubinadamu.

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka akimfariji mtoto Yohana Lyanga alipomtembelea hospitalini hapo kwa lengo la kujua hali yake.

Aidha, amebainisha kuwa Serikali itagharamia matibabu ya mtoto huyo hadi pale hali yake itakapoimarika, pamoja na kugharamia matibabu hayo, Mkuu huyo wa Wilaya  ameahidi kuwa Serikali itamlea mtoto huyo, itamsomesha na kumpatia huduma zitakazohitajika.

Naye, Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Mtakatifu Joseph kilichopo Dumila Wilayani Kilosa Dkt. Selemani  Sakoro amethibitisha kumpokea mtoto huyo Agosti 29 akiwa na majeraha sehemu za makalio na kubainisha kuwa hali yake kwa sasa inaendelea vizuri.

Tukio la Mtoto Yohana Lyanga limetokea katika Kata ya Msowelo Wilayani Kilosa ambapo alikuwa anaishi na ndugu zake akiwemo shangazi na Mjomba wake ambapo hadi sasa tayari shangazi na baba wa mtoto huyo wanashikiliwa na Jeshi la Polisi katika kituo cha Polisi cha Dumila kwa ajili ya mahojiano zaidi.

 

Bi. Caroline Makemo mlezi wa Kituo cha watoto yatima kilichopo Dumila amejitolea kumuhudumia mtoto huyo hospitalini hapo.

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka akiwa pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya hiyo wakifanya mahojiano na watuhumiwa wa ukatili katika Kituo cha Polisi Dumila.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.