• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO AMSHUKURU RAIS KUTOA ZAIDI YA BIL. 21 KUBORESHA SEKTA YA AFYA.

Posted on: October 19th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Abubakar Mwassa amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zaidi ya shilingi Bil.21 kwa lengo la kuboresha Sekta ya Afya Mkoani humo fedha ambazo zimeelekezwa kwenye ujenzi na ukarabati wa majengo ya kutolea huduma ya Afya.

Fatma Mwassa amemshukuru Rais Oktoba 19,2022 mara baada ya kutembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa huo ili kujionea mwenyewe ujenzi wa majengo mbalimbali yanayojengwa katika Hospitali hiyo pamoja na kuona huduma za Afya zinazotolewa kwa wananchi zinazotolewa na Hospitali hiyo.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Morogoro Dkt. Daniel Nkungu akiwatambulisha madaktari wa hospitali hiyo kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwassa wakati wa ziara fupi hospitalini hapo.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa mwaka huu wa fedha kupitia Halmashauri za Mkoa huo imetoa jumla ya Shilingi 18 Bil. kwa ajili ya kuboresha huduma za Afya huku Hospitali ya Mkoa ikipokea Shilingi Bil. 3 kwa ajili ya ujenzi wa majengo na ukarabati achilia mbali fedha zilizotolewa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya Hospitali.

Muonekano wa jengo jipya  la wagonjwa mahututi (ICU) katika hospitali ya Rufaa  Morogoro.

“Lakini nitumie fursa hii kwa niaba ya wananchi wote wa Morogoro kumshukurusa sana mama yetu mpendwa Rais wa awamu ya sita Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutupa upendeleo wa kipekee wanamorogoro kutuletea fedha nyingi za huduma za Afya kuboresha huduma za Afya katika Mkoa wetu” amesema Fatma Mwassa.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwassa akimsikiliza Mganga Mfawidhi Dkt. Daniel Nkungu walipotembelea jengo la  kuhudumia  watoto njiti lililopo hospitalini hapo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwassa akiwa katika chumba cha CT-Scan kujionea namna mashine hiyo inavyofanya kazi.

Akiongea mbele ye vyombo vya habari mesema, hospitali hiyo imeboreshwa kwa kiasi kikubwa na huduma zinazotolewa kwa sasa ni za uhakika huku akitumia fursa hiyo kuwajulisha wananchi uwepo wa kipimo cha CT-Scan ambapo kwa mara ya kwanza imeletwa na Serikali ya awamu ya sita tangu kuanzishwa kwake mwaka 1946, hali inayowapunguzia wananchi gharama ya kusafiri nje ya Mkoa huo kutafuta kipimo hicho.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro akipanda mti mbele ya jengo la wagonjwa wa dharura wakati wa ziara yake hospitalini hapo.

Aidha, amesema hali ya upatikanaji wa dawa katika hospitali hiyo kwa sasa ni asilimia 98 hii ni kutokana na juhudi zinazofanywa na Serikali ya awamu ya sita katika kuboresha huduma za Afya hapa nchini.

Katika hatua nyingine Kiongozi huyo amewataka wananchi wa wa Mkoa huo kupata matibabu ya awali katika Vituo vya Afya na zahanati vinavyopatikana katika maeneo yao kwa lengo la kupunguza foleni na gharama zisizo za lazima na kwamba lengo la uwepo wa Hospitali ya rufaa ni kuwahudumia wagonjwa waliopewa Rufaa kutoka maeneo mengine.

Mkuu wa Mkoa akisalimiana na wananchi waliokuwa wanasubiri huduma katika hospitali hiyo ya Rufaa Morogoro.

Lakini pia ametumia fursa hiyo kuwakumbusha wananchi wa Mkoa huo kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya iliyoboreshwa (iCHF) ili kupunguza gharama za matibabu pindi wanapougua kwa kujiunga pamoja na kupata Bima hiyo kwa gharama nafuu.

Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Morogoro Dkt. Daniel Nkungu amesema, pamoja na ujenzi wa majengo mengine hospitali hiyo inajenga jengo la kuchuja damu ambalo litawahudumia wagonjwa wenye matatizo ya damu na kuongeza kuwa kwa sasa huduma ya Watoto njiti inapatikana kutokana na uwepo wa jengo la kuwahudumia Watoto hao.

Muonekano wa jengo la huduma za dharura katika hospitali ya Rufaa Morogoro.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kusirye Ukio amesema kuwa hospitali hiyo ya Rufaa inamahusiano mazuri na hospitali nyingine za binafsi ikiwemo hospitali ya Mtakatifu Francis iliyopo Ifakara Wilaya ya Kilombero Mkoani huo mahusiano ambayo yanahusisha pia kuwapeleka wataalamu kujifunza huduma ya mama na mtoto lengo ni kupunguza vifo vinavyotokana na uzazi.


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kusirye Ukio akizungumza na watumishi wa hospitali hiyo kwenye kikao na Mkuu wa Mkoa Fatma Mwassa.

Miongoni mwa miradi inayoendelea kutekelezwa Haospitali ya Rufaa ni pamoja na ujenzi wa jengo la huduma za dharura ambalo ujenzi wake umekamilika, jengo la wagonjwa mahututi linasubiri kukabidhiwa kutoka kwa mkandarasi, jengo la uchujaji wa damu ambalo lipo hatua za mwisho, jengo la Watoto njiti pamoja na miundombinu ya umeme.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.