• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO AMSHUKURU RAIS SAMIA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA MKOANI HUMO.

Posted on: June 14th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima amemshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha huduma za Afya kwa Wananchi wa Morogoro na Tanzania kwa ujumla kwa kutoa fedha za kujenga vituo vya Afya na Hospitali za Wilaya.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akiwa na viongozi mbalimbali wakati akikagua ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Gairo.

Mhe. Adam Malima ametoa pongezi hizo Juni 12 mwaka huu wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Gairo ikiwa ni muendelezo wa ziara yake kwa Halmashauri zote Tisa za Mkoa huo lakini pia kushiriki mabaraza ya Madiwani kwa ajili ya kusimamia kujibu hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali - CAG.

Akiwa katika Hospitali hiyo Mkuu wa Mkoa amefurahishwa na huduma zinazotolewa hospitalini hapo hivyo akawataka Wahe. Madiwani wa Halmashauri hiyo na nyingine kuwa mabalozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuyasema hayo mazuri yanayofanywa na Serikari ya awamu ya sita.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akimpa pole mtoto Devoth Julius (5) anayepata matibabu katika hospitali ya Wilaya ya Gairo baada ya kuumia Mguu wake akiendesha baiskeri.

"...Dkt. Samia amepeleka x- Ray kama hizi na hapa nimezikuta kama hizo zinafanya kazi, unajua sio kiini macho...sasa haya ndo mambo ambayo Mwenyekiti wa Madiwani mnawajibika kuyasema, kweli kabisa..." amesema Mkuu wa Mkoa.

Akiongelea suala la maji Wilayani humo Adam Malima amesema suala la maji ni changamoto kubwa kwa Gairo na inatakiwa kupatiwa ufumbuzi haraka.

Hapa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima anasikiliza kero ya uhaba wa maji kwa baadhi ya  wanawake waliokuwa wanachota maji kwenye moja ya bomba Wilayani Gairo.

Kwa sababu hiyo ameiagiza Mamlaka ya Maji Safi na usafi wa Mazingira Wilaya ya Gairo (GAUWASA) kuhakikisha wanakamilisha upatikanaji wa maji kwa wakazi hao ndani ya miezi mitatu kwa kutumia njia mbalimbali ikiwemo ya kuchimba visima virefu na au kupata maji kwa njia ya mseleleko.

Moja ya mtambo wa kisasa wa kuchimbia visima virefu vya maji pamoja na mafundi wakiendelea na zoezi la uchimbaji wa visima vya maji katika eneo la Kisitwi Wilayani Gairo.

Hapa Mkuu wa Mkoa pamoja na viongozi mbalimbali wakiwa kwenye eneo ambalo uchimbaji wa visima vya maji unaendelea.

Sambamba na hayo Mhe. Adam Malima akiwa kwenye kikao cha Baraza la Madiwani aliitaka Halmashauri hiyo kukusanya mapato kwenye sekta ya mifugo kwani amesema Sekta hiyo inakusanya 6% tu makusanyo ya ndani kupitia ushuru wa machinjio na ushuru wa  mifugo wakati Sekta ya kilimo inakusanya mapato kwa 34% hivyo kuitaka Sekta hiyo iwe na mikakati ya ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri.

Picha mbalimbali za Wahe. Madiwani wakati wa Kikao.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Makame amepongeza kasi ya Mkuu wa Mkoa katika utendaji kazi wake na kuahidi kuwa katika mwaka wa fedha 2023/2024 wanakwemda kukusanya zaidi ya bilion moja ya mapato yasiyolindwa.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Makame (kulia) akimueleza jambo Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Mipango na Uratibu Bwa. Anza - Ameni Ndosa.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Rachel Nyangasi amebainisha changamoto mbalimbali zinazoikabili Halmashauri yao kuwa ni pamoja na upungufu wa vyombo vya usafiri jambo linalochangia kushuka kwa mapato na kuwa na miradi kutokamilika kwa wakati sababu ya ufuatiliaji mdogo unaosababishwa na uhaba wa vyombo vya usafiri.

Wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Gairo Mhe. Rahel Nyangasi akiwa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro wakati wa Kikao Cha Baraza la Madiwani.

Nae Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi - CCM tawi la Kisitwi Bw. Godson Ngunei amemuomba Mkuu wa Mkoa na viongozi wengine wa chama na Serikali kuunga mkono juhudi za Wananchi waliochangia ujenzi wa nyumba ya mganga wa zahanati ya Kisitwi ili iweze kukamilika kwa wakati, aidha, Mwenyekiti huyo amemshukuru Mkuu wa Mkoa na viongozi alioambatana nao kwa lengo la kukagua miradi ya maendeleo.

Mkuu wa Mkoa alikagua miundombinu ya barabara Wilayani Gairo.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.