• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO AMSHUKURU RAIS SAMIA KUSOGEZA HUDUMA YA AFYA KWA WANANCHI

Posted on: June 3rd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwasogezea karibu wananchi huduma za kibingwa kwa kupeleka madaktari bingwa katika ngazi ya Wilaya ili kuwapunguzia gharama wananchi wasio na uwezo wa kufuata huduma za Afya katika hospitali za Rufaa.

Mhe. Adam Malima amebainisha hayo Juni 3, 2024 alipokutana na madaktari Bingwa 35 maarufu kama Madaktari Bingwa wa Dkt. Samia Suluhu Hassan baada ya kuripoti Mkoani humo tayari kuaza majukumu ya kuwahudumia wananchi wa Mkoa huo ukiwa ni mpango kabambe wa Mhe. Rais Samia wa kutaka Halmashauri zote 184 hapa nchini kufikiwa na madaktari hao Bingwa na kutoa huduma za kibingwa kwa wananchi.

Mhe. Malima amesema, nje ya mpango huo, Serikali ya Mama Samia imefanya kazi kubwa katika sekta ya Afya kwani hadi sasa imepunguza vifo vinavyotokana uzazi kutoka vifo 556 kwa mwaka 2015/2016 hadi 104 mwaka 2021/2022 kwa kila Wanawake 100000 sawa na asilimia  81, hii ni kwa mujibu wa ripoti ya viashiria vya afya ya uzazi (TDHS).

"... kuanzia miaka ya 2015 hadi 2020 tumetoka kwenye vifo 556 kwa kila akinamama 100,000 hadi 2022 kuwa na vifo 104 ni sawa na asilimia 81..." amesema Mhe. Adam Kighoma Malima

Sambamba na hilo,  Mhe. Adam Malima pamoja na kuwapongeza madaktari Bingwa kwa kufanya kazi kubwa ya kuokoa uhai wa watu, amewataka kuendelea kutoa elimu ya lishe na chakula bora kwa wananchi, kwani amesema kuna uzalishaji mkubwa wa chakula kwa maeneo mengi ya Mkoa huo  lakini bado elimu hiyo haijaenea kwa wananchi, hivyo amewataka kutoa elimu ya ulaji wa vyakula bora unaozingatia makundi yote ya vyakula.


Katika hatua nyingine, Waziri wa Katiba na Sheria Balozi Pindi Chana, aliyekuwepo katika tukio hilo muhimu la kuwapokea madaktari hao, alipopewa nafasi ya kusema neno kwa wananchi kutokana na jambo hilo kubwa analolifanya Dkt. Samia, amempongeza Rais Samia kwa kuongeza bajeti ya Sekta ya Afya huku akiwataka wananchi kuwa na utamaduni wa kupima afya zao mara kwa mara kama wanavyofanya check up ya vyombo vyao vya moto kila baada ya muda hivyo hivyo kwa mwanadamu badala ya kusubiri kuumwa ndipo uende hospitali.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Wizara ya Afya Dkt. Ismail Mtitu amesema mpango huo ni wa wiki nane ambapo ulizinduliwa Mei 6, Mwaka huu Mkoani Iringa na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu (Mb) ambapo huduma hizo za kibingwa zitafikiwa hospitali zote 184 za Halmashauri zote za Mikoa 26 ya Tanzania Bara na kila Halmashauri itapokea madaktari bingwa 5 ili kutoa huduma za kibingwa kwa wagonjwa wa idara ya nje na ndani katika hospitali husika.

Nae, Dkt. Joyce Gimonge ambaye ni Daktari Bingwa wa Watoto kutoka Mkoani Geita, kwa niaba ya madaktari wenzake amesema wananchi wanapaswa kuwahi matibabu mapema pale wanapohisi kuumwa ili kupata vipimo na kupewa matibabu ya haraka na hivyo kuokoa maisha yao.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.