• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO ANENA MWAKA MMOJA WA RAIS SAMIA.

Posted on: July 3rd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amemshukuru Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuweza kuwaondolea wananchi wa Mkoa huo kero ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa kipindi hiki kifupi Cha Uongozi wake.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akitoa salam za pongezi kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Kongamanp la wadau wa Elimu wa Mkoa huo Julai 2 Mwaka huu katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kiislam cha Morogoro (MUM) Mkoani humo.



Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Bi. Mariam Mtunguja akimkaribisha Mkuu wa Mkoa huo ili azungumze na wadau wa elimu katika Kongamano hilo.

Martine Shigela amesema hayo Julai 2 mwaka huu katika kongamano la wadau wa elimu la kufanya tathmini ya sekta ya Elimu na kumpongeza Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Kiislam cha Morogoro.


Mhe. Palamagamba Kabudi Mbunge wa Jimbo la Kilosa akizungumza wakati wa kutoa pongezi hizo.

Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albart Msando akiteta jambo na Mwenyekiti wa Chama Tawala Mkoa wa Morogoro Ndg. Doroth Mwamsiku wakati wa Kongamano hilo.

Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha kuwa kipindi cha mwaka mmoja wa uongozi wa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ni cha mafanikio makubwa kwenye Sekta mbalimbali hapa nchini hasa katika Sekta ya maji ambapo zaidi ya shilingi 8bil. zimetumika kwa mwaka wa fedha wa 2021/2022 katika ujenzi miradi ya kimkakati inayolenga kuwaondolea kero hiyo wananchi wa Mkoa wa Morogoro.


Katibu Tawala Msaidizi upande wa Elimu wa Mkoa huo Bi. Germana Mung'aho akisoma taarifa ya uwepo wa wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari Mkoani Morogoro.



Zawadi zilizoandaliwa kwa ajili ya Halmashauri, Shule na Wanafunzi waliofanya vizuri kitaaluma Mkoani Morogoro.

Aidha, ameongeza kuwa Miradi ya maji inayotarajiwa kujengwa katika miji 28 nchini kote, Mkoa wa Morogoro ni mnufaika wa mradi mmojawapo utakaotekelezwa Katika Mji Mdogo wa Ifakara  ambapo ukamilikaji wake utachangia kwa kiasi kikubwa kukomesha kabisa kero ya Maji kwa wakazi wa maeneo hayo.



“Kwa mwaka wa fedha ulioisha ni zaidi 8Bil. zimetumika katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maji Mkoa mzima kama sehemu ya kusogeza huduma kwa wananchi” amesema Shigela.

“Na zaidi ya Tsh. 50Bil. zimetengwa kuanza kujenga mradi mkubwa wa maji katika Hamashauri ya Mji mdogo wa Ifakara ambapo ni moja ya miradi inaotarajiwa kutekelezwa katika Miji 28 nchi nzima” ameongeza Shigela.

Katika hatua nyingine Martine Shigela ameweka wazi kuwa kwa upande wa elimu bila malipo Mkoa wa Morogoro kwa kipindi cha mwaka mmoja umepokea zaidi ya 14Bil. kuweza kugharamia elimu bila malipo kwa Shule za Msingi na Sekondari.



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akipokea zawadi ya usimamizi bora na kama mdau mkubwa wa elimu kutoka kwa Katibu Tawala wa Mkoa huo Bi. Mariamu Mtunguja pamoja na Katibu Tawala Msaidizi upande wa Elimu Mkoa wa Morogoro Bi. Germana Mun'gaho.

Naye Mwenyekiti wa Chama Tawala CCM Mkoa wa Morogoro Ndg. Doroth Mwamsiku amesema Chama hicho Mkoani humo kinafurahishwa na mwenendo wa utendaji wa walimu katika kuendelea kuwapatia maarifa watoto wa Kitanzania ili kujenga taifa lililobora na lenye utashi.


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Morogoro Ndg. Doroth Mwamsiku akiwasilisha salam za chama wakati wa Kongamano la wadau wa elimu la Kumpongeza Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Nao wadau wa kada hiyo akiwemo Mwalimu Mipiana Donard Kilasile ambaye ni Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Lukwiva ametoa wito kwa walimu na watendaji wengine kusimamia na kufuatilia vema ufundishaji wa watoto ili kuweza kufikia malengo ya kuinua Mkoa huo kielimu.


Mwalimu Mipiana Donard Kilasile ambaye ni Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Lukwiva akizungumza mara baada ya Kongamano la wadau hao.




Baadhi ya wadau wa elimu Mkoani Morogoro wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Mkoa huo akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela.



MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.