• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO ASISITIZA USHIRIKIANO KATIKA KUTUNZA VYANZO VYA MAJI

Posted on: February 12th, 2025


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima, amewataka wadau wa maji Mkoani humo na wanamorogoro kwa ujumla, kushirikiana katika kutunza vyanzo vya maji vinavyopatikana Mkoani humo kwa ajili ya kizazi hiki na vizazi vijavyo.

Mhe. Adam Malima amebainisha hayo wakati wa kikao cha wadau wa maji Mkoani humo kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Morena iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.


Amesema, miaka 50 iliyopita, idadi ya watu ilikuwa milioni 15 na rasilimali za maji zilitosha mahitaji ya wananchi, kwa sasa idadi ya watu imeongezeka hadi milioni 65, hivyo kumeongeza mahitaji ya maji kwa matumizi ya shughuli za kibinadamu na kutaka ushirikiano katika kutunza vyanzo vya maji.


"...Miaka 50 iliyopita nchi nzima kulikuwa na watu milioni 15 ambapo maji yalitosheleza sasa wapo watu zaidi ya milioni 65, hivyo kumekuwa na uhitaji wa maji, tunapaswa kushirikiana, kulinda na kutunza vyanzo vyetu kuepuka vita ya maji siku zijazo..."


Pamoja na ukweli kuwa Mkoa wa Morogoro ni moja ya mikoa yenye utajiri mkubwa wa vyanzo vya maji, huku Bwawa la Kidunda likitajwa kuwa litakuwa mhimili mkuu wa nishati ya umeme hapa nchini, bado amewataka wanasiasa kutoingilia masuala msingi ya rasilimali maji, ili kuhakikisha uhifadhi wa vyanzo vya maji unalindwa.


Katika hatua nyingine, Mhe. Malima amewaagiza Wakurugenzi Watendaji wa Halmashuri zote za Mkoa huo kulipa kipaumbele suala la kulinda vyanzo vya maji na kulifanya kuwa ajenda namba moja katika vikao vyote vya kisheria wanavyovifanya katika maeneo yao.


Sambamba na hayo, Mhe. Adam amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya maji ili kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama kwani wananchi zaidi ya milioni 3.6 wa Morogoro wanategemea upatikanaji wa maji bora kwa matumizi yao ya kila siku.


Awali, Mkurugenzi msaidizi wa sera, tafiti na ubunifu wa Wizara ya Maji Bw. Alex Tarimo akitoa salamu kwa niaba ya Katibu Mkuu  kutoka Wizara hiyo amesema mwaka 1960 upatikanaji wa maji kwa kila mtu ulikuwa wa meta za ujazo 12600 hadi kufikia 2025 hali ya upatikanaji wa maji umekuwa meta za ujazo 1980, hivyo amewasisitiza wadau wa maji na mazingira kushirikiana kulinda na kuendeleza vyanzo hivyo vya maji.


Kwa upande wake, Meneja wa RUWASA Mkoa wa Morogoro Mhandisi Sospeter Lutonja amesema kikao hicho kimeitishwa mahsusi kwa ajili ya kutathmini miradi iliyotekelezwa ili utekelezaji huo uweze kufikia 85% kama ilani ya Chama cha Mapinduzi inavyoelekeza.


Naye Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Wami - Ruvu Elibariki Mmasy amesema, katika Mkoa wa Morogoro, bodi hiyo imefanya utafiti maeneo ya Manispaa ya Morogoro na kubaini uwepo wa akiba ya maji lita 34,000, huku eneo la Dakawa likiwa na kiasi cha kati ya lita 10,000 hadi 93,000.


Katika bajeti ya mwaka 2024/2025 serikali imetoa Tsh. Bil. 16 kwa ajili ya miradi ya maji lengo ni kumtua Mama ndoo kichwani.


Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.