• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Morogoro ataka migogoro ya ardhi, wakulima na wafugaji ikomeshwe

Posted on: September 28th, 2023

RC morogoro ataka migogoro ya ardhi, wakulima na wafugaji ikomeshwe.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amewaagiza wakuu wa Wilaya wote Mkoani humo kufanya tathmini ya Migogoro ya Ardhi katika maeneo yao na kuratibiwa na wakurugenzi ikiwa ni hatua za kukabilana na migogoro hiyo.

Mhe, Malima ametoa maaagizo hayo Septemba 27, mwaka huu alipofanya kikao na wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Mkuu wa Mkoa huyo amesema kuwa yeye sio kwamba anapinga ufugaji bali anapenda kuona ufugaji wenye tija kwa Mkoa huo na sio ufugaji holela unaosababisha migogoro.

“watakwambia kwamba Mkuu wa Mkoa wa Morogoro akataa Mifugo Morogoro Subhanallah naanzia wapi, mifugo inayofungwa na kuratibiwa vizuri ni uchumi mkubwa sana kwa Mkoa wa Morogoro lakini mifugo ambayo hairatibiwi ni disaster (janga) kwa Mkoa wa Morogoro” amesema Malima

Aidha, Mhe. Adam Malima amewataka viongozi hao Kwenda kuandaa mapendekezo ya mabadiliko ya sheria ndogo zitakazotumika kulipa faini kwa mifugo itakayoharibu mazao ili kukomesha kabisa migogoro ya wakulima na wafugaji mkoani humo kwani amesema kiwango cha faini kinachotumika sasa hakina uhalisia ukilinganisha na thamani ya fedha zinazolipwa kama fidia ya mazao yanayoharibiwa na mifugo hiyo.

Maagizo mengine aliyoyatoa Mkuu huyo ni Pamoja na kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ukusanyaji wa mapato ya ndani, kusimamia mikopo ya asilimia kumi kukopeshwa kwa vikundi vinavyotambulika na kufanya ufuatiliaji na kurejesha fedha hizo kwa wakati.

Sambamba na maagizo hayo amewataka Wakuu wa Wilaya kuweka mikakati ya kukomesha migogoro ya kutengenezwa ndani ya wilaya zao kwa kuwa amesema hakuna migogoro inayoshuka kutoka angani isipokuwa migogoro hiyo inatengenezwa na kuwataka watu hao watafutwe na kuwajibishwa lakini pia amewataka wakuu hao kuweka mazingira wezeshi ya kujiandaa kwa kilimo cha mazao ya kimkakati.

Katika juhudi za kuimarisha na kupunguza migogoro ya wakulima na wafugaji mkoani humo Mshauri wa Jeshi la Akiba Mkoa wa Morogoro Kanali Valentine Makyao amebainisha mikakati aliyo nayo ya kutembelea kila Halimashauri za MKoa  huo ili aweze kuboresha mafunzo ya jeshi hilo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mhe, Sebastian Waryuba kwa niaba ya Wakuu wa Wilaya za Mkoa huo amemshukuru Mkuu wa Mkoa na kukiri kuyapokea maelekezo aliyoyatoa na kwamba yatatekelezwa kama ambavyo ameagiza.

Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.