• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Morogoro ateua Kamati kuhakiki eneo la ujenzi wa Sekondari Wilayani Mvomero

Posted on: March 12th, 2022

RC MOROGORO ATEUA KAMATI YA KUKAGUA ENEO SALAMA LA KUJENGA SEKONDARI KATA YA HOMBOZA WILAYANI MVOMERO.

 

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela ameteua Kamati ya watu saba kwa ajili ya kukagua eneo la kujenga Sekondari ya Kata ya Homboza iliyopo Wilayani Mvomero baada ya eneo la awali lililokuwa limekubaliwa kujenga Sekondari hiyo kujiridhisha kuwa sio salama kwa wanafunzi watakaosoma shule hiyo.

Martine Shigela ameteua Kamati hiyo Machi 11 mwaka huu alipofanya ziara mahususi kwa ajili ya kuokoa fedha zaidi ya Shilingi milioni 470 zilizotolewa na Serikali na kutofanyiwa kazi kwa zaidi ya miezi miwili kwa sababu ya mivutano ya wapi shule hiyo ijengwe.

Kwa sababu hiyo Martine Shigela amefika kijiji cha manza Kata ya Homboza Wilayani Mvomero ambapo shule hiyo inatakiwa kujengwa ili kujiridhisha kama kuna mgogoro wa Ardhi unaochelewesha ujenzi wa shule hiyo na kujiridhisha mbele ya wananchi wa kijiji cha Manza kuwa hakuna mgogoro wowote wa Ardhi na kwamba kama kuna mwananchi ana mgogoro na eneo hilo aende mahakama.

“Yako maeneo masaa yote ni mgogoro tu, hata Ardhi isiyokuwa na mgogoro wanataka watengeneze mgogoro, na wengine wanataka Ardhi sio kwa ajili ya kujiendeleza, wanataka wachukue ili wakauze kwa watu wengine” amesema Martine Shigela.

“Kwa hiyo suala la Ardhi tumefunga, Kamishna wa Ardhi kama kutatokea mgogoro mwingine mwambie aende mahakamani” RC Shigela amesisitiza.

Katika Hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa ameteua Kamati ya kwenda kukagua eneo ambalo limekubaliwa na wananchi kujenga shule ya sekondari baada ya eneo la awali kuonekana kutofaa ujenzi huo kwa kuwa ni chepe chepe na hatarishi kwa wananafunzi watakaosoma shuleni hapo.

Wajumbe hao ambao wamepewa siku mbili ya kufanya kazi hiyo na kutakiwa  kuwasilisha taarifa yao kwa Mkuu wa Mkoa hapo Machi 14 mwaka huu ni pamoja na Afisa Elimu wa Mkoa wa Morogoro, Afisa Mazingira wa Mkoa, Kamishna wa Ardhi wa Kanda ya Mashariki na Afisa Elimu wa Wilaya ya Mvomero.

Wajumbe wengine wa Kamati hiyo ni Afisa Tarafa ya Mlali na Afisa Ardhi wa Wilaya ya Mvomero  wote wameagizwa kuambatana na Diwani wa Kata ya Homboza Hamidu Bakari Kalungwana kupitia eneo ambalo wananchi wameliteua kuwa mbadala wa eneo la awali ili kuona endapo eneo hilo linafaa kwa ujenzi huo ama la na kama halitafaa basi Kamati hiyo itafute eneo jingine lisilo na mgogoro wowote.

Wananchi wa Kijiji cha Manza wakiongozwa na Diwani wao Mhe. Mamidu Bakari Kalungwana amethibitisha kuwa eneo hilo halina mgogoro na uvumi kuwa eneo hilo lina mgogoro umetungwa tu na baadhi ya wananchi wasioitakiwa mema Serikali yao ambao muda wote wanatamani kuchochea vurugu.

Mhe. Kalungwana amesema wao walipendekeza eneo la awali kwa baada ya kuona lina nafasi kubwa zaidi ya Ekari 40 na kwamba shida kubwa ya eneo hilo ni mto ambapo kunatakiwa kujengewa kivuko na wao walikuwa tayari kujenga kivuko hicho hata hivyo wameshukuru maelekezo yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa na kwamba wataungana na timu iliyoundwa ili kupata mwafaka wa suala hilo.

Kwa upande wake Sikitu Shomari Mkazi wa Kijiji cha Manza amekubaliana na maelekezo yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa ya kuunda kamati itakayopitia maeneo yote ili kupata eneo linalokidhi vigezo vya kujenga Sekondari yao huku Hamis Somba akimshukuru Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha za kujenga sekondari ya watoto wao hivyo itapunhguza umbali wa Km zaidi ya 40 kufika shule waliyokuwa wanasoma awali.

Kwa upande wake Ndugu Simbamwene mwananchi wa kijiji cha Manza ambaye pia ndiye alijitolea eneo la ujenzi wa shule ya Sekondari amemuomba Mkuu wa Mkoa kupitia Kamati aliyoiunda kuendelea kufanya utafiti zaidi kuhusu eneo la awali kwa kuwa anaamini eneo hilo ni salama, changamoto yake ni kutokuwepo kwa karavati jambo ambalo anasema wananchi wanaweza kulijenga karavati hilo.

Machi 10 mwaka huu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – TAMISEMI alifanya ziara ya siku moja ambapo pamoja na mambo mengine alifika katika Kijiji cha Manza na kukagua eneo la ujenzi wa shule hiyo ya sekondari na kutoa maelekezo kuwa eneo hilo sio salama kwa wanafunzi kwa kuwa ni eneo lenye maji maji na kutaka litafutwe eneo jingine.

Serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepeleka shilingi milioni 470 katika Kata ya Homboza na baadae inatarajiwa kupeleka shilingi milioni 130 kwa ajili ya ujenzi Sekondari kuanza kujenga vyumba nane vya madarasa, jengo la utawala, Maabara na majengo mengine ujenzi ambao umecheleweshwa na mivutano ambayo tayari imekwishatatuliwa na Mkuu wa Mkoa.


MWISHO

 

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.