• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Morogoro atoa onyo kwa wafanyabiashara wa saruji

Posted on: November 23rd, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare amewataka waafanyabiashara wa Saruji Mkoani humo kuacha maramoja kupandisha bei ya saruji na badala yake kuuza bidhaa hiyo kwa bei ya awali kwa kuwa Serikali imejiridhisha hakuna sababu ya msingi ya kupandisha bei huku akiwaonya kuwa atakayekiuka agizo hilo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Loata Ole Sanare ametoa agizo hilo leo Novemba 23 mbele ya waandishi wa habari alipokutana na wafanyabiashara wa bidhaa hiyo Ofisini kwake na kuzungumzia hali ya bei ya bidhaa hiyo kabla na baada ya kupanda na kutoa maagizo yaSerikali.

Amesema, kabla ya bei ya saruji kupanda, Wilaya zilizopembeni mwa Mkoa wa Morogoro hususan za mbali kama Ulanga,  bei ya Saruji mfuko mmoja ulikuwa unauzwa shilingi 15,000 hadi 16,000 na sasa ni shilingi 16,500 hadi 19,000, Wilaya ya Malinyi kabla bei kupanda mfuko mmoja uliuzwa shilingi 16,000 hadi 19,000 na sasa ni shilingi 16,500 hadi 20

.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa ameshangazwa na bei ya saruji kuuzwa kwa bei ya juu zaidi katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kuliko hata Wilaya za mbali ambapo mfuko mmoja kabla ya kupanda uliuzwa shilingi 13,000 hadi 18,000 na sasa bei ya bidhaa hiyo inapatikana kwa shilingi 15,500 hadi 25,000 jambo ambalo amesema kufanya hivyo ni sawa na kuihujumu Serikali.

Kwasababuhiyo,Loata Ole Sanare amewaagiza wafanyabishara wote Mkoani humo kuunza saruji bei isiyozidi shilingi 16,000 kwa mfuko na atakayekiuka agizo hilo atachukuliwa hatua kali za kisheria kwa sababu Serikali imejiridhisha hakuna sababu zozote za msingi za kupandisha bei ya saruji.

                                               

“Na kwa maana hiyo bei ya saruji itaendelea kuwa ileile bei ya awali….elfu kumi na tatu na mia tano kama ilivyokuwa awali na isizidi elfu kumi na sita, tumejiridhisha, hakuna sababu yoyote ambayo ni genuine (msingi) inayofanya bei ipande” .amesema Loata Sanare.

Aidha, amewashauri wafanyabiashara hao kuwa kama kuna sababu yoyote inayowafanya wapandishe bei ya saruji, nivema wakaijengea hoja sababu hiyo na kuiwasilisha Ofisi ya Mkuu wa Mkoa naye ataiwasilisha hoja hiyo kwa viongozi wa juu ikiwemo Wizara husika.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewaagiza Maafisa waTRA Mkoa wa Morogoro kuwakagua wafanyabiashara wa saruji waliouza saruji zaidi ya shilingi 16,000/= kwa mfuko mmoja wapigiwe hesabu na kulipa fedha ya mapato ya ongezeko hilo la bei.

Nao wafanyabiashara wa saruji Mkoani humo walipohojiwa na vyombo vya habari juu ya ongezeko la beiwametoasababumbalimbalihukuBw. Thabiti Mohamed Islam akisema ongezeko hilo limetokana na uhaba wa bidhaa hiyo kiwandani kwa kuwa wateja wameongezeka hususan wakutoka nchi jirani ikiwemo Kenya na Jamhuri ya Kideokrasia ya Kongo ambako viwanda vyake vya Saruji vimefungwa kutokana na COVID – 19.

           

Hata hivyo Bw. Thabiti Mohamed ameishauri Serikali kutoruhusu wafanyabiashara wa nchi jirani kuchukua saruji hapa nchini ili bidhaa hiyo ipatikane kwa urahisi na hivyo kuzuia ongezeko la bei hiyo.

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.