• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Morogoro atoa siku 11.

Posted on: January 21st, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare ametoa siku 11 kwa Wenyeviti wa Mtaa na viongozi wengine wa Mji Mdogo  wa Mikumi kusimamia zoezi la michango  kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari Mikumi na kukamilisha michango hiyo  kabla au ifikapo Januari 31 mwaka huu.

Loata Sanare ametoa agizo hilo januari 19 mwaka huu katika ukumbi wa Mikutano wa VETA Mikumi wakati wa ziara yake ya siku moja katika Mji huo kwa ajili ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa vinne vinavyotakiwa kujengwa katika shule hiyo.

Aidha, Loata Sanare amewataka viongozi hao wahakikishe kila mwananchi anayestahili kutoa mchango anachanga kwa ajili ya ujenzi wa Shule hiyo kabla ya tarehe tajwa vinginevyo sheria kali dhidi yao zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kutiwa mbaloni.

Mkuu huyo wa Mkoa amewataka watendaji hao kutomuogopa mtu yoyote katika utendaji wao huku akisisitiza kutoa taarifa kwa mamlaka husika iwapo kunajitokeza hali ya uvunjaji wa sheria za kazi.

’’Acheni kuwa na nidhamu ya woga, wanakimbia kimbia kwa sababu Mkuu wa Wilaya anakuja, wanakimbia kimbia kwa sababu Mkuu wa Mkoa anakuja msifanye kazi kwa hali hiyo, fanyeni kazi kwa uadilifu fanya kazi kwa utaratibu unaotakiwa huna sababu ya kumuogopa mtu ’’ amesisitiza Sanare.

Akizungumzia suala la mapato katika Mji huo, Loata Sanare amebainisha kuwa wanahitajika watu waadilifu katika ukusanyaji wa mapato ili kusaidia kutekeleza shughuli za maendeleo katika Mji huo.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare  ametembelea Shule ya Msingi Mikumi Mpya iliyopo katika mji huo na kubaini upungufu wa madawati na vyumba vya madarasa kwa wanafunzi wa Shule hiyo.

Hali hiyo imebainishwa pia na Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Ibrahim Chemba aliyekiri kuwepo kwa changamoto hiyo ambapo amesema  inapelekea kupungua kwa ufanisi wa ufundishaji kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi kukaa chini na kubanana wakati wa kujifunza.

Kutokana na hali hiyo, Loata Sanare amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa kumhamisha Shule Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Mikumi Mpya Ibrahim Chemba kutokana na kushindwa kuwa mbunifu katika kutatua changamoto za shule yake.

‘’Tafuta Shule nyingine,  miaka mitano inakutosha hukutusaidia shule hii, ninakutoa kwenye Ualimu Mkuu kwa sababu umeshindwa kuwa mbunifu’’ amesema Loata.

Wakati huo huo wanafunzi wa Shule hiyo akiwemo Havintishi Juma ameiomba Serikali kutatua changamoto ya madawati na vyumba vya madarasa kutokana na kukaa wanafunzi zaidi ya 100 katika darasa moja.

Emmanuel Lazaro ambaye ni Mkazi wa Mikumi, ametaja changamoto inayopelekea wazazi kushindwa ujenzi wa miundombinu ya shule kuwa ni pamoja na dhana ya Elimu bure ambayo baadhi ya wazazi hushindwa kuielewa na kuitafisiri kuwa Serikali inafanya kila kitu bila kuwashirikisha wazazi.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.