• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Morogoro awasweka ndani wenyeviti 21, amshusha cheo Mkuu wa Shule asitisha likizo ya Mtendaji.

Posted on: January 6th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare amemuagiza Mkuu wa Polisi Wa Wilaya ya Kilosa kuwaweka rumande wenyeviti 21 wa Vitongoji katika Mji mdogo wa Mikumi Wilayani humo kwa kushindwa kuhamasisha wananchi kushiriki ujenzi wa vyumba vinne vya madara yanayohitajika kwa ajili ya wanafunzi 200 waliofaulu mitihani ya darasa la saba mwaka 2020 na kutarajia kuanza masomo yao January 11 mwaka huu katika Shule ya Sekondari ya Mikumi.

Loata Sanare ametoa agizo hilo January 6 mwaka huu wakati wa ziara yake ya Siku tatu kukagua utekelezaji wa agizo la Serikali lililotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa la kutaka Wanafunzi wote waliofaulu mitihani ya darasa la saba 2020 kuwa madarasani mara Shule zitakapofunguliwa hivyo kila Mkoa umetakiwa kuhakikisha Wanafunzi hao hawakosi vyumba vya madarasa ya kusomea wala Madawati ya kukalia.

Hali ilikuwa sio ya kuridhisha sana Loata Sanare alipofika Shule ya Sekondari ya Mikumi ambapo wanafunzi 432 wamepangiwa katika Shule hiyo huku Wanafunzi  200 Kati yao kuonekana Kukosa vyumba vya madarasa manne huku kukiwa hakuna jitihada za makusudi  zinazochukuliwa katika kukamilisha ujenzi huo hususan kwa wenyeviti wa Vitongoji wa Mji Mdogo wa Mikumi katika kuhamasisha wananchi, kushiriki ujenzi huo ambao bado uko hatua ya Msingi huku zikiwa zimebaki Siku tano tu kwa Shule zote kufunguliwa na Wanafunzi kuanza masomo yao na kuamua kutoa agizo hilo.

"...Hatukubaliani naye kabisa, OCD watendaji wote 21 ukimuondoa huyu  niwakute wote kesho wapo ndani na wakija hapa watafanya Kazi ya kusomba wenyewe si wanashindwa kuwahamasisha watu wao, watakuja kushiriki wenyewe". ... amesema Sanare.

Aidha katika ziara hiyo Loata Ole Sanare amemuagiza Afisa Elimu wa Mkoa huo Eng. Joyce Baravuga kumuachisha nafasi ya Ukuu wa shule Mkuu wa shule ya Sekondari ya Kauzeni Mwl. Exavery Makaranga iliyoko katika Manispaa ya Morogoro kwa kutoonesha jitihada za dhati za kuendeleza ujenzi wa vyumba vya Maabara ambavyo vina zaidi ya miaka 13 bila kukamilika huku yeye akiwepo hapo kwa zaidi ya mika sita.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Kauzeni Exavery Makaranga ambaye amesimamishwa nafasi ya Ukuu wa Shule hiyo.

Akiwa katika eneo la Shule hiyo Mkuu huyo wa Mkoa pia amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Sheilla Lukuba  kumrudisha Mara moja Mtendaji wa Kata ya Kauzeni Jenipha Rashid ambaye yuko nyumbani kwa likizo na matazizo ya kifamilia kurudi Kazini Mara moja ili kuendelea na usimamizi  wa Ujenzi wa vyumba vya madarasa wanavyodaiwa kwa ajili ya wanafunzi waliofaulu.

Mkuu wa Mkoa Loata Ole Sanare yuko katika ziara ya Siku tatu katika Wilaya za Morogoro, Kilosa, Kilombero na Malinyi kwa ajili ya kukagua utekelezaji wa agizo la Serikali hususan ujenzi wa vyumba vya madarasa.

MWISHO.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.