• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Morogoro awataka Ma DC kusimamia Miradi ya Kimkakati.

Posted on: June 21st, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigella amewataka Wakuu wa Wilaya walioapa viapo vyao leo kuweka vipaumbele katika miradi ya kimkakati iliyoanzishwa Mkoani humo ili kuuletea Mkoa huo maendeleo ya haraka.

Shigella ametoa maagizo hayo kwa wakuu wa Wilaya hao Juni 21, mwaka huu katika viwanja vya Ikulu ndogo Mjini Morogoro wakati wa kuwaapisha Wakuu wa Wilaya watano walioteuliwa hivi karibuni na Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha, Shigella amebainisha baadhi ya Miradi hiyo ya Kimkakati kuwa ni pamoja na Sehemu ya  ujenzi wa kipande cha Reli ya mwendokasi – SGR  kinachojengwa ndani ya Mkoa huo na  mradi wa umeme wa Bwawa la Mwalimu Nyerere  ambao hadi sasa upo katika hatua nzuri ya kukamilika.

Katika hatua nyingine, Shigela amewataka ma DC hao kuwafuata wananchi katika maeneo yao  kwa lengo la  kusikiliza na kutatua kero wanazokumbana nazo ili kuuweka Mkoa huo katika hali ya usalama na kuleta maendeleo ya wananchi wake.

‘’Kero zipo nyingi sana na nyingine zimechukua muda mrefu sana bila kutatuliwa, kwanza tujenge misingi ya kuwasikiliza wananchi wanaolalamika na tusikilize watu wenye majibu ili tupime kati ya mlalamikiwa na mlalamikaji nani yupo sahihi’’ amesema Shigella.

June 18 mwaka huu, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania alifanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya nchini ambapo katika Mkoa wa Morogoro aliwateuwa Wakuu wa Wilaya watano ambao ni Jabil Makame (Gairo), Hanji Godigodi (Kilombero) na Halima Okashi (Mvomero).

Wengine walioteuliwa na Mhe. Rais na kuapishwa leo na Mkuu wa Mkoa huo wa Morogoro ni Albert Msando (Morogoro) na Majid Mwanga (kilosa) huku waliobakizwa kuendelea na majukumu ya Ukuu wa Wilaya zao za awali ni Mathayo Francis Maselle na Ngollo Ng’waniduhu Malenya wa Wilaya ya Ulanga.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.