• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO AWATAKA VIONGOZI KUELEKEZA NGUVU ZAO KULINDA MAZINGIRA

Posted on: November 3rd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa amewataka viongozi Mkoani humo kuunganisha na kuelekeza nguvu zao katika kulinda Mazingira katika maeneo wanamoishi. Mhe. Fatma Mwassa ametoa agizo hilo Novemba 3 mwaka huu, kwenye kikao kazi cha viongozi wa Mkoa na Wilaya kilichofanyika katika ukumbi wa Magadu Katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Mkuu wa MKoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa (katikati) akiongoza Kikao Kazi cha viongozi wa ngazi ya juu kabisa ndani ya Mkoa huo wakiwemo viongozi wa Kamati za Ulinzi na Usalama ya Mkoa na Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya zote za Mkoa huo. Kushoto kwake ni Katibu Tawala wa Mkoa huo Dkt. Mussa Ali Mussa.

Mkuu wa Mkoa amesema Mkoa huo unashika nafasi ya nne katika uzalishaji wa chakula hapa nchini, hivyo ikiwa mazingira ya Mkoa huo yataharibiwa wakulima hawataweza kulima na kupata mazao kwa kiwango kile ambacho nchi inatalajia. “...nasema hivi, suala la mazingira ni letu sote... ‘no compromise’...” amesema Fatma Mwassa.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa (katikati waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamona na Wakuu wa Wilaya wa Mkoa huo na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa baada ya Kikao cha Viongozi wa Mkoa na Wilaya.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa (katikati waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na Sekretarieti ya Mkoa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa baada ya kikao cha Mkuu wa Mkoa na Viongozi wa Mkoa na Wilaya.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ametaja athari zinazotokana na uharibifu wa mazingira zikiwemo upungufu wa maji katika mto Ruvu ambao unatokana na uharibifu mkubwa wa mazingira katika mikoa ya Pwani na Morogoro ambao unatokana na uwepo wa shughuli za kibinadam zinazoendelea katika vyanzo vya maji. Sambamba na hilo, Mhe. Fatma Mwassa amesema wafugaji wanaolisha mifugo yao kwenye mashamba ya wakulima wanatakiwa kuchukuliwa hatua kali kwa mujibu wa kisheria.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Kwa upande wao wajumbe wa kikao hicho Alhaj Majid Mwanga ambaye pia ni Mkuu  wa Wilaya ya Kilosa ameshauri  kuwatumia Maafisa Tarafa katika ukusanyaji wa mapato, kutatua migogoro ya wafugaji na wakulima na hata kuleta mahusiano mazuri kati ya wananchi na Serikali yao kwa kuwa wao ni kiungo muhimu sana katika ustawi wa maendeleo ya Taifa letu.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Makame amesema msingi mkuu wa utekelezaji wa maazimio yote ya kikao hicho ni mahusiano mazuri na mshikamano wa viongozi wa Mkoa, Wilaya, Halmashauri na wananchi kwa ujumla, hivyo changamoto zote zinazowakabili wananchi zitatatuliwa kwa wakati.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.

Wakurugenzi watendaji wa Halmashauri wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Fatma Mwassa.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.