• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Morogoro awataka wataalamu kupeleka huduma ya Umeme, Maji na Barabara Kituo cha Afya Kinonko

Posted on: September 27th, 2021

RC Morogoro awalalia macho Mameneja, Kituo cha Afya Kinonko.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amemuagiza Meneja wa Shirika la Umeme  - TANESCO Mkoa wa Morogoro Mhandisi Fedgrace Shuma kufikisha huduma ya Umeme katika Kituo cha Afya cha Kinonko kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro ili kurahisisha kituo hicho kuanza kutoa huduma ya Afya kwa wananchi wa eneo hilo kabla au ifikapo mwezi Disemba mwaka huu.

Martine Shigela ametoa agizo hilo Septemba 27 mwaka huu akiwa katika ziara ya siku moja ya kukagua utekelezaji wa miradi ya Maendeleo na kusikiliza kero za wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro ikiwemo ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kinonko kilichopo katika Tarafa ya mikese.

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Gwata, Mkuu wa Mkoa Martine Shigela  amesema Serikali imeleta fedha za kujenga majengo matano ya kituo hicho cha Afya sio kwa ajili ya kupendezesha watu au kwa ajili ya matumizi mengine bali yamejengwa ili kutoa huduma ya Afya kwa wananchi.

Aidha amefafanua kuwa wakati fedha hizo zinaletwa wakati wa erikali ya awamu ya tano Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati huo akiwa Makamu wa Rais alikuwa anamkumbusha mara kwa mara aliyekuwa Rais wakati huo na kipenzi cha watanazania hayati John Pombe Joseph Magufuli namna akina mama walivyokuwa wanapata tabu wakati wa kujifungua.

Kwa sababu hiyo, Mkuu wa Mkoa huyo amesema hakubaliani kukamilika kwa majengo hayo matano huku yakiwa hayatoi huduma ya Afya kwa sababu tu ya kukosekana kwa Umeme, Maji au Barabara na akatumia fursa hiyo kuagiza Meneja wa TANESCO Mkoa wa Morogoro na wataalamu wa Maji na Barabara kupeleka huduma hizo katika Kituo hicho cha Afya.

 ‘’… Na mimi nakubaliana na maelezo ya Mhe. Diwani umeme, maji na barabara yetu lazima iwe ndo kipaumbele chetu cha kwanza kuhakikisha kituo chetu kinafunguliwa haraka …’’ alisisitiza Martine Shigela.

“….haiwezekani Rais Samia atuletee fedha tukamilisha majengo haya, halafu sisi ambao tuliopewa dhamana ya kusaidia mambo madogo madogo haya yatushinde, haiwezekani”. Alisisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Kwa upande wa changamoto ya maji,  Shigela amesema tayari Wakala wa Maji Mijini na Vijini - RUWASA pamoja na kuwa na mpango wa muda mrefu wa kusambaza maji katika kata hiyo ikiwemo Kituo hicho cha Afya, badoimetafuta imetenga  Shilingi Milioni 30 kwa ajili ya kuchimba kisima cha maji ambacho kitasaidia kufikisha maji kituoni hapo na kutatua kero hiyo kwa muda hivyo amemuagiza Meneja wa RUWASA Wilaya  ya Morogoro Mhandisi Grace Lyimo kukamilisha mradi huo haraka ili kituo hicho kianze kutoa huduma kwa wananchi.

Akizungumzia suala la barabara, Shigela amesema hadi sasa Serikali ya Mhe. Samia Suluhu Hassan imetenga kiasi cha Shilingi Bilioni 1.5 kwa mwaka huu wa fedha 2021/2022 kwa ajili ya ujenzi wa barabara katika Halmashauri ya Morogoro ukilinganisha na fedha Tsh. Mil. 200 zilizokuwa zimetengwa katika bajeti ya mwaka 2020/2021 hivyo zitasaidia kujenga miundombinu ya barabara ikiwemo ya kuelekea kituo cha Afya cha Kinonko.

Diwani wa Kata ya Gwata Zongo lobe Zongo, amesema Kituo hicho cha Afya kinategemewa na wananchi kutoka Kata hiyo na kata nyingine za jirani hivyo kukamilika kwake kutasaidia kupunguza umbali mrefu wanaotembea wananchi wake na wa kata za jirani waliokuwa wanafuata huduma za Afya katika kata  nyingine za Halmashauri hiyo.

Sambamba na hayo, Zongo amemuomba Mkuu wa Mkoa, kuwasaidia wananchi wa kata hiyo kutatua changamoto ya kutokuwa na mtandao wa simu ili kuondoa adha ya mawasiliano wanayokumbana nayo wananchi  wake katika kuwasiliana na ndugu, jamaa na marafiki na kusaidia kuwarahisishia wananchi kwenye masuala ya kiuchumi.

Nao wananchi akiwemo Mariam Abdallah wa Kata ya Gwata amesema kutokuwepo kwa huduma ya umeme, maji na ubovu wa barabara  katika kituo chao cha  Afya cha Kinonko kumepelekea hadi sasa kituo hicho kushindwa kufanya kazi hivyo changamoto hizo kuzidi kuwarudisha nyuma kimaendeleo.

Mradi wa Kituo cha Afya Kinonko ulianza Septemba 2019 kwa gharama ya Shilingi Milioni 400 ikiwa ni ujenzi wa majengo matano ambayo ni jengo la nyumba ya mtumishi, jengo la kuhifadhia maiti, jengo la Maabara, jengo la upasuaji na jengo la mama na mtoto.

 Mradi wa Kituo cha Afya cha Kinonko Katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro ulianza Septemba 2019 kwa gharama ya Shilingi Milioni 400 ikiwa ni ujenzi wa majengo matano ambayo ni jengo la nyumba ya mtumishi, jengo la kuhifadhia maiti, jengo la Maabara, jengo la upasuaji na jengo la mama na mtoto.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.