• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO AZINDUA RASMI MICHEZO YA MEI MOSI, ATOA NENO.

Posted on: April 20th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa amezindua rasmi michezo ya Mei Mosi ikiwa ni maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ambayo kitaifa itafanyika Mkoani Morogoro.

Wakati wa uzinduzi huo Mhe. Fatma Mwassa amewataka Wakuu wa Taasisi za Serikali na Waajiri wa sekta nyingine hapa nchini, kuwaruhusu Wafanyakazi wao kushiriki michezo hiyo pamoja na kutenga bajeti kwa ajili ya maadhimisho ya Mei Mosi ijayo.

Fatma Mwassa ametoa Ushauri huo leo Aprili 20 mwaka huu wakati wa uzinduzi huo ambapo pia amekagua timu mbalimbali za michezo tayari kwa kuanza mashindano hayo ambayo yanafanyika uwanja wa Jamhuri uliopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema kumekuwa na tabia ya baadhi ya Wakuu wa Taasisi na Waajiri kutowaruhusu watumishi wao kushiriki michezo wakati wa maadhimisho hayo kwa kisingizio cha ukosefu wa fedha, hivyo amewaomba waajiri wote pamoja na Taasisi za Serikali kutoa msukumo kwenye suala la michezo kwa kuwa michezo inajenga Afya, utimamu wa mwili, kuongeza tija kazini na kuimarisha mahusiano baina ya wafanyakazi.

“...naomba kuwakumbusha Viongozi watenge bajeti kwa ajili ya michezo na pia watenge muda kwa wafanyakazi wao kufanya michezo, kwa kufanya hivyo wafanyakazi watakuwa na utimamu wa mwili na kuongeza tija kazini...” amesema Mhe. Fatma Mwassa.

Nae Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amesema Maadhimisho ya Mei Mosi huambatana na michezo mbalimbali kwa lengo la kuonesha umuhimu wa wafanyakazi kuwa pamoja na kuimarisha Afya za Wafanyakazi.

Kwa upande wao washiriki wa michezo hiyo akiwemo Kocha wa timu ya kuvuta kamba kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Bw. Nikasi Luanda amesema wamekuja kutetea ubingwa wao kwenye mashindao haya kwa kuwa mashindano yaliyopita ambayo yalifanyika Mkoani Dodoma waliibuka washindi wa kwanza kwa upande wa Wanawake na Wanaume na wanaamini mwaka huu pia watakuwa mabingwa kwa michezo hiyo.

Kilele cha Maadhimisho ya Mei Mosi Kitaifa mwaka huu yatafanyika Mkoani Morogoro katika uwanja wa Jamhuri, Mgeni rasmi wa maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Kauli mbiu ya Mei Mosi mwaka huu ni “Maslahi Bora, Mishahara juu, kazi iendelee” wakati kaulimbiu ya Michezo ya Mei Mosi inasema “Miaka miwili ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeimarisha michezo na kuongeza ufanisi kazini, Kazi iendelee”.

 


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • MAFUNZO YA AMIS NA TAUSI YATOLEWA MKOANI MOROGORO.

    May 21, 2025
  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.