• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MWASSA AAHIDI USHIRIKIANO KUKUZA MICHEZO MKOANI MOROGORO

Posted on: April 12th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa ameipongeza Taasisi ya Fountain Gates Schools kwa kuonesha nia ya kuwekeza katika michezo Mkoani Morogoro na kuahidi kutoa ushirikiano ili kuhakikisha kuwa nia hiyo inatimia.

Mhe. Mwassa ameyamesema hayo Aprili 12, 2023 wakati akiwapongeza wachezaji na viongozi wa timu ya wanawake ya Fountain Gates ambayo imechukua ubingwa wa kombe la Afrika kwa mashindano ya Shule za Sekondari mwaka 2023 baada ya kukutana na Mkuu huyo wa Mkoa Ofisini kwake.

Mhe. Fatma Mwassa amesema anaipongeza Taasisi ya Fountain Gates kwa wazo la kuweka kituo cha michezo Mkoani Morogoro kwani amebainisha kuwa kufanya hivyo kutaibua na kuendeleza vipaji vya watoto hususani wakike na kukuza soka la wanawake hapa nchini.

 “...kubwa lililo tufurahisha zaidi ni nia ya Fountain Gate ya kuwekeza katika Sports Accademy hapa kwetu Morogoro, tunawakaribisha sana na tupo tayari kushirikiana nanyi....na tutahakikisha ndoto yenu inatimia...” amesema.

Sambamba na hilo Mkuu huyo wa Mkoa ameipongeza timu hiyo kwa kutwaa ubingwa wa Mashindano ya shule za Sekondari barani Afrika kwa upande wa wanawake huku wakitoa mchezaji bora wa mashindano hayo, mfungaji bora na kipa Bora hivyo amewapongeza viongozi wa timu hiyo kwa kujitoa kwao, kuiandaa timu hiyo hadi kutwaa ubingwa huo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wakuu wa Shule za Fountain Gates Tanzania Bw. Joseph Mjingo amesema mafanikio wanayoyapata ni kutokana na sera nzuri ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan husuan katika utekelezaji mzuri wa Mtaala wa elimu na michezo kwa kuifanya michezo kuwa sehemu ya vipindi darasani.

Nae, Naodha wa timu hiyo Felista Richard amesema ushindi walioupata ni kutokana na ushirikiano kutoka Serikalini na kujituma kwao uwanjani huku akiiomba Serikali kutoa fursa kwa vijana kuonesha vipaji vyao ili waweze kuyafikia malengo waliojiwekea.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.