• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MWASSA ATAKA MOROGORO IWE SAFI

Posted on: September 10th, 2022

RC Morogoro, atamani Morogoro iwe safi 

USAFI WA MAZINGIRA NI JUKUMU LETU SOTE, MIFUMO IFANYE KAZI – FATMA MWASSA

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Aboubakar Mwassa amesema anatamani mazingira ya Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro yawe safi ili kuepusha magonjwa ya mlipuko na kuipunguzia Serikali mzigo katika kupambana na maadui watatu ambao ni Ujinga, maradhi na umaskini.

Fatma Mwasa ametoa kauli hiyo Septemba 10 mwaka huu wakati akizindua Kampeni ya usafi wa Mazingira katika halmashauri yua Manispaa hiyo alipoungana na wananchi wengine kufanya usafi wa mazingira katika Kata za Mji Mkuu, Sultani area pamoja na mitaa mingine ya mji huo na kutoa maagizo ya Serikali.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Fatma Mwassa (aliyevaa kofia pana) akifanya usafi wa Mazingira katika kata ya Sultani area, Septemba 10 mwaka huu

Fatma Mwassa ambaye katika uzinduzi huo amekuja na Kaulimbiu inayosema USAFI NI JUKUMU LETU SOTE, MIFUMO IFANYE KAZI, amesema nia yake kubwa ni kutaka Manispaa hiyo iwe safi huku akiagiza Mifumo ya Kiserikali yote kwa maana ya Ofisi au Watendaji wake kuwajibika kufanya kazi hiyo bila kusukumwa.

“Langu ni moja tu, kwamba lazima Morogoro iwe safi, lazima tutunze mazingira Morogoro, tumeanza na kampeni ya usafi kusafisha mazingira lakini kampeni inayuofuata ni ya kupanda miti kila nyumba, na miti hiyo itakuwa ni angalau ya matunda” ameagiza Fatma Mwassa.

Maelekezo mengine ya Kiserikali ambayo yametolewa na kiongozi huyo ni pamoja na kila mwananchi kufanya usafi wa mazingira katika mazingira yanayomzunguka kila siku, na siku ya Jumamosi usafi huo utafanywa kwa pamoja kwa kila mtaa kuanzia asubuhi hadi saa nne na maduka au biashara zitafunguliwa baada ya usafi huo kufanyika.

Aidha, ameagiza kuwa kila Jumamosi ya kwanza ya mwezi kutakuwa na usafi mkubwa utakaoambatana na ukaguzi na kulipa faini kwa wale ambao hawatawajibika kufanya usafi katika maeneo yao huku akiwatahadharisha wananchi kutii sheria bila shuruti na kwamba sheria ndogo zinazohusu usafi wa mazingira kama zilikuwa hazitumiki zianze kufanya kazi yaani kulipa faini ya shilingi 50,000/= kila kosa moja la aina hiyo.

Katika Hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewageukia watendaji wa Serikali wakiwemo Watendaji wa Kata na maafisa Afya ambao hawatasimamia ipasavyo Usafi wa Mazingira katika maeneo yao ya kazi watapewa onyo au kuchukuliwa hatua za kinidhamu kama hawatarekebisha utendaji wao wa kazi hata baada ya kuonywa.

Kwa maneno mengine Mkuu huyo wa Mkoa katika uzinduzi huo hakuridhika na usafi wa mazingira ya Manispaa ya Morogoro, kwa sababu hiyo kazi hiyo ameiacha mikononi mwa Watendaji wa Serikali wakiwemo Watendaji wa Mitaa, Kata, Afya na kuwataka kila mmoja katika ngazi yake na eneo lake atomize wajibu wake kwa kutumia neno fupi tu, MIFUMO IFANYE KAZI.

“usafi wa mazingira ni jukumu letu sote, mifumo ifanye kazi”

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.