• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Shigela aagiza kuukarabati mnara wa mashujaa

Posted on: July 25th, 2022

RC Shigela aagiza kuukarabati mnara wa mashujaa

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela ameielekeza Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kuukarabati mnara wa Mashujaa uliopo katika Halmashauri hiyo uweze kufanana na kumbukumbu ya historia ya Mashujaa waliopigania uhuru katika nchi hii.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro  Martine Shigela ( wa kwanza kushoto) akiwa pamoja na kamati ya  ulinzi na usalama wakati wa maadhimisho ya siku ya mashujaa ambayo yamefanyika katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Julai 25 mwaka huu.

Shigela ametoa agizo hilo Julai 25 mwaka huu wakati wa maadhimisho ya siku ya Mashujaa yaliyofanyika eneo la Mnara wa mashujaa uliopo eneo la Posta katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa lengo la kuwakumbuka mashujaa hao waliopambana wakati wa harakati za ukombozi wa Taifa la Tanzania na Afrika kwa jumla.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela  akielekeza Mnara huo kufanyiwa ukarabati wa haraka

Martine Shigela amesema kuwa Historia ya Mashujaa waliopigania uhuru wa nchi ya Tanzania ni muhimu kutunzwa na kuhifadhiwa vema ili vizazi vijavyo viweze kujifunza na kuelewa vema historia ya Taifa na bara la Afrika.

“Nielekeze kuanza mara moja harakati za kuukarabati Mnara huu kwa kuupaka rangi, kuweka vema Majina ya Mashujaa na kuwasha taa juu ya kilele cha mnara huu ili kuwaenzi mashujaa wetu” ameagiza Shigela.

Aidha, Martine Shigela amesema suala la uzalendo na ushujaa kila mmoja anaweza kulionesha kwa namna yake kulingana na sehemu yake ya kuwajibika ili kuendelea kuitunza amani iliyopo, pamoja na kuliletea maendeleo taifa la Tanzaia.


Baadhi ya wafanyakazi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro pamoja na wananchi wa Halmashauri hiyo wakifanya usafi katika Mnara wa Mashujaa kama sehemu ya kuwakumbuka Mashujaa hao leo Julai 25 mwaka huu.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando amekitaka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kuendeleza vema maeneo na kufufua viwanda ambavyo viliachwa katika Tawi la Chuo hicho lililopo Mazimbu ili kuwaenzi Mashujaa hao kwa kufanya kazi za maendeleo ya kijamii.


Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando akiweka shada la maua katika mnara huo wakati wa Maadhimisho hayo.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro akiweka shada la maua kama ishara ya kuwakumbuka Mashujaa.


Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi Fortunatus Musilimu ambaye ni Kamanda wa Jeshi hilo Mkoani  Morogoro akiwakilisha Kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa huo kuweka shada la maua katika Mnara wa Kumbukumbu ya Mashujaa.


Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Mhe. Pascal Kihanga amebainisha kuwa wamepokea maelekezo yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa na kwamba ukarabati wa Mnara huo utafanyika mara moja kwa lengo la kuwaheshimisha Mashujaa hao.


Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga akiahidi kupokea na kuyafanyia kazi maelekezo ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kwa kuyatekeleza kwa wakati.

Siku ya Mashujaa huazdhimishwa hapa nchini kila mwaka ifikapo Julai 25 ili kuwakumbuka mashujaa hao walipigania ukombozi wa Taifa la Tanzania na Afrika kwa ujumla, ambapo kwa mwaka huu, maadhimisho hayo kitaifa yamefanyika Mkoani Dodoma katika viwanja vya Mashujaa.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.