• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC SHIGELA AWAAHIDI USHIRIKIANO WAKUFUNZI WA SENSA NGAZI YA MKOA.

Posted on: July 26th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amewaahidi ushirikiano Wakufunzi wa sensa ngazi ya Mkoa waliohitimu mafunzo yao leo Julai 26 na kuwataka kwenda kufanya kazi kwa weledi ili kufanikisha zoezi hilo kwa ufanisi.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akimkabidhi zawadi ya cheti cha kuhitimu Mafunzo mmoja wa washiriki wa Mafunzo ya Makarani Wakufunzi wakati wa kufunga mafunzo hayo Julai 26 mwaka huu katika Chuo cha WAMO Mkoani Morogoro.




Martine Shigela amesema hayo Julai 26 mwaka huu wakati wa kufunga Mafunzo ya wakufunzi hao ambapo pamoja na mambo mengine amewataka wakufunzi hao kwenda kuandaa Makarani na Wasimamizi kwa kuzingatia weledi, sheria na kanuni ili kupata Makarani na Wasimamizi makini wa kufanya zoezi hilo.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akihutubia Makarani Wakufunzi wakati wa kufunga Mafunzo hayo.



Aidha, Martine Shigela amebainisha kuwa, zoezi la sensa ya watu na Makazi litafanyika Agosti 22 kuamkia Agosti 23 mwaka huu hivyo kwa wananchi ambao hawatafikiwa na Makarani wa sensa siku hiyo wasipate hofu wowote kwani watafikiwa na Makarani hao ndani ya siku sita kuanzia tarehe tajwa hapo juu ambapo wataulizwa taarifa za wananchi waliolala katika Kaya zao siku ya kuamkia Agosti 23, 2022.




Martine Shigela amebainisha kuwa Kamati ya Sensa ya Mkoa wa Morogoro ina imani kubwa na wakufunzi hao kwani wao pamoja na Makarani na Wasimamizi wa zoezi hilo ndio taswira haswaa ya zoezi la sensa kwa kukusanya takwimu sahihi zitakazosaidia Serikali kuweka mipango yake Katika kutoa huduma stahiki kwa wananchi.

“Kwa hiyo tuna imani kubwa na Ninyi, mtakwenda kufundisha Makarani watakaofanya kazi yao kwa uadilifu na kujituma, tunaamini mtakwenda kutuletea taarifa zenye ubora unaotakiwa” amebainisha Shigela.

Sambamba na hayo, Martine Shigela amewataka wakufunzi hao kuuwakilisha vema Mkoa wa Morogoro kwa kutembelea maeneo yao ya kazi mapema zaidi ili kurahisisha zoezi hilo wakati wa ukusanyaji wa taarifa.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando kwa niaba ya Wakuu wa Wilaya wa Mkoa huo amesema, Halmashauri za Wilaya Mkoani humo zipo tayari kupokea mafunzo kutoka kwa Wakufunzi hao kwani ndio matumaini yao kwao ya kuwapiga msasa Makarani na Wasimamizi watakaokwenda kwa wananchi wakati wa zoezi la sensa.


Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kuhutubia wahitimu wa mafunzo ya Makarani Wakufunzi.



Kwa upande wake Bw. Athumani Kapate ambaye ni mmoja wa Makarani Wakufunzi ameishauri jamii kuacha tabia ya kuficha watu wenye ulemavu na kusababisha kutokuhesabiwa kitendo kinachopelekea kundi hilo Maalum kukosa haki zao za msingi, hivyo ameishauri kuwapa haki kundi hilo ili kuhesabiwa.


Kamati ya Sensa ya Mkoa wa Morogoro ikiwa katika picha ya pamoja baada ya kufungwa kwa mafunzo hayo.


Baadhi ya Wahitimu wa Mafunzo ya Makarani wakufunzi kutoka Halmashauri za Mkoa wa Morogoro wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro na Viongozi wengine baada ya kufungwa kwa mafunzo hayo.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.