• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC SHIGELA AMPONGEZA NA KUMSHUKURU RAIS KWA KUDUMISHA AMANI, UMOJA

Posted on: March 19th, 2022

RC SHIGELA AMSHUKURU RAIS KWA KUDUMISHA AMANI, UMOJA 

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kudumisha Amani na Umoj wa Taifa hilo huku akibanisha kuwa kwa kipindi kifupi cha siku 365 ameuonesha Ulimwengu kuwa Tanzania ni nchi inayoendesha siasa za kistaarabu.


Umati wa wananchi walioshiriki sherehe za mwaka mmoja wa Mhe. Samia Suluhu Hassan kuwa madarakani, uwanja wa Jamhuri Mjini Morogoro


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela (wa pili kushoto) na Katibu wa Chama cha Mapinduzi (wa pili kulia) wakiingia Uwanja wa Jamhuri wakati wa maadhimisho hayo

Martine Shigela ametoa pongezi na shukrani hizo Machi 19 mwaka huu wakati wa sherehe za maadhimisho ya Mwaka mmoja tangu alipoaapa kuwa Rais wa Tanzania sherehe ambazo kimkoa zimefanyika Uwanja wa Jamhuri uliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema, tangu Mhe. Samia Suluhu Hassan ashike kijiti hicho cha kuliongoza Taifa la Tanzania yapo mambo makubwa yamefanyika ndani ya kipindi kifupi ikiwa ni pamoja na kuudhihirishia Umma wa Tanzania na Dunia kwa jumla namna Taifa la Tanzania limeendelea kuwa Taifa lenye Umoja, Amani, Mshikamano na Upendo, na kuonesha ukomavu wa Kidemokrasia kwa kuwasamehe baadhi ya Watanzania waliokuwa wamewekwa vizuizini kwa makosa mbalimbali.



Katibu wa CCM Mkoa wa Morogoro akiteta jambo na Mwenyekiti wa Chama hicho Mkoa wa Morogoro Mhe. Dorothy John (kulia)

“Rais wetu ameudhihirishia Umma wa Watanzania na Dunia kwamba Taifa letu limeendelea kuwa Taifa lenye Umoja, Mshikamano, Amani na Upendo, kazi hii ameifanya vizuri, ameonesha Ukomavu wa Kidemokrasia hata wale ambao wamewekwa ndani amekwenda kuwasamehe”  amesema Martine Shigela.

Ameongeza kuwa, Baadhi ya Nchi kiongozi mmoja anapomaliza muda wa uongozi wake au kufariki wananchi wake huingia kwenye matatizo makubwa kwa sababu ya baadhi ya viongozi  kugombania madaraka hali ambayo hata hupelekea umwagaji damu, tofauti na demokrasia na siasa za Tanzania huku akitolea mfano wa tukio la kifo cha Rais John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea Machi 17, 2021 tukio ambalo limepita kwa amani na utulivu.




Akizungumzia mafanikio ya Mhe. Samia Suluhu Hassan yaliyopatikana katika kipindi chake amesema Mkoa wa Morogoro yapo mengi yaliyofanyika ikiwa ni pamoja na kupokea zaidi Shilingi Billioni 11 fedha za Elimu bila Malipo.

Aidha, amebainisha kuwa shilingi Bilioni 30 zimetolewa na Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa Miundombinu ya Elimu ambapo zaidi ya Maboma 302 yamekamilishwa na Madarasa 849 yamejengwa kwa kutumia pesa za Uviko 19.


Pamoja na mafanikio hayo amesema bado Serikali hiyo ilitoa shilingi Bilioni 19, ndani ya Mwaka mmoja huo huo na kujenga Shule Mpya 23 kama sehemu ya kuinua Elimu ya ngazi mbalimbali ndani ya Mkoa huo.

Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha kuwa, katika Sekta ya Afya ndani kwa kipindi cha mwaka mmoja cha Mhe. Samia Suluhu Hassan amejenga zaidi ya zahanati 29 kwa gharama ya shilingi Bil. 42, huku Sekta ya Maji ikipewa zaidi ya shilingi bilioni 186 ambapo Mkandarasi yupo mbioni kuanza kazi za ujenzi wa kuwapatia wananchi wake maji safi, salama na tosherevu.

Kuhusu umeme Vijijini Mkuu huyo wa Mkoa amewaagiza Wakuu wa Wilaya pamoja na Viongozi ngazi ya Kata kufuatilia na kusimamia utekelezaji wa zaidi ya bilioni 52 zilizoletwa na Mhe. Rais Samia kwa ajili ya kufikisha nishati ya umeme zaidi ya vijiji 260.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Morogoro Bi. Doroth  Mwamsiku amesema, Chama kupitia ngazi zake za Tawi, Kata, Wilaya na Mkoa wamesimamia Miradi yote iliyotajwa na kuwahakikishia Wananchi kwamba miradi hiyo imekamilika kwa ufanisi mkubwa na kwa kiwango cha hali ya juu.


Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro Mhe. Dorothy John

Wakizungumza katika sherehe hizo kwa niaba ya Wakuu wa Wilaya wengine, Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Majid Mwanga wamesema Mwaka mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan umekuwa ni mwaka wa mafanikio makubwa na umefungua na kurahisisha shughuli za kiuchumi katika maeneo mbalimbali ya Wilaya hizo.



Mkuu wa WilayayaMorogoro Albert Msando

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Majid Mwanga



Akitoa salamu za shukrani Meya wa Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga amesema kuwa, Manispaa ya Morogoro inamshukuru Mhe. Rais Samia kwa kufanikisha Shughuli mbalimbali za Miradi ya Maendeleo ikiwa ni pmoja na kufanikisha Mkopo wa Shilingi bilioni 1 kwa ajili ya shughuli za Mipango Miji zitakazotumika katika Upimaji wa Viwanja zaidi ya 1,500  ndani ya Manispaa hiyo.


Meya wa Manispaa ya Morogoro Mhe. Pascal Kihanga



MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.