• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC SHIGELA APOKEA ZAWADI YA RAIS SAMIA

Posted on: April 20th, 2022

RC MOROGORO APOKEA ZAWADI YA RAIS SAMIA

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amepokea zawadi ya picha ya kuchorwa ya Rais Samia Suluhu Hassan kutoka kwa Msanii Mboya Hosiana kutoka Wilaya ya Gairo Mkoani humo akimtaka Kiongozi huyo afikishe picha hiyo kwa Rais.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Matrine Shigela (mwenye kaunda suti) akiwa katika picha ya pamoja na Msanii wa kuchora picha pamoja na Wakuu wa Wilaya za Mkoa huo na viongozi wengine wa Chama na Serikali. kulia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro Doroth John


Shigela amepokea picha hiyo kutoka kwa msanii Hosiana Aprili 20 mwaka huu ikiwa ni alama ya kumuunga Mkoano Samia Suluhu Hassan Raisa Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani kwa jitihada zake za kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia filamu ya Royal Tour inayoonesha vivutio vya utalii nchini ambayo imezinduliwa hivi karibuni katika ukumbi wa Guggenheim Museum ulioko mjini New York nchini Marekani.

RC Shigela akipokea picha kutoka kwa Msanii wa kuchora picha Mboya Hosiana (kulia)




Pamoja na Mkuu wa Mkoa kuahidi kuifikisha zawadi hiyo kwa Rais kama alivyoombwa na msanii huyo, amepomngeza Msanii kwa kutumia kipaji chake kuonesha uzalendo kwa nchi yake na kwa kumuunga mkono Rais na kumzawadia shilingi milioni moja za kitanzania (Tsh. 1,000,000.00).

Mboya Hosiana akikabidhiwa kitita cha shilingi milioni moja kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela ikiwa ni pongezi za kumuunga Mkono Mhe. Samia kwa jitihada zake za kutangaza Utalii wa Tanzania 

Aidha, Martine Shigela ameongelea jitihada zinazofanywa na Rais Mhe. Samia Suluhu  Hassan za Kutangaza vivutiao vya Tanzania kuwa kazi hiyo ni ya manufaa kwa nchi huku akibainisha kuwa tayari jitihada hizo zimekwisha anza kuzaa matunda kwa hifadhi za taifa zilizoko Mkoani humo kwa kuongeza watalii wanaotembelea hifadhi hizo na kwamba baadhi yake zimeshavuka lengo  ikiwemo mbuga ya taifa ya Mikumi ambayo imevuka kwa asilimia 20.

“Na juzi nimetembelea kule wamenieleza kuwa mwaka huu peke yake baada ya Rais kufanya jitihada zile wameshavuka lengo la mwaka mzima kwa zaidi ya asilimia ishirini” amebainisha Martine Shigela.

Akiongea baada ya kukabidhi zawadi hiyo ya picha kwa Mkuu wa Mkoa na kupokea zawadi ya shilingi milioni moja, Msanii huyo amesema ameamua kumpa zawadi hiyo Rais ili kusaidia kampeni aliyoiazisha ya kutangaza vivutio vya Utalii vilivyopo hapa nchini na ambapo sasa vimeanza kujulikana Duniani kote.

Msanii wa Kuchora picha Mboya Hosiana kutoka Wilaya ya Gairo akiwa na picha aliyoichora

hii ndiyo picha ambayo imechorwa na Msanii Mboya Hosiana na kuomba imfikie Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama zawadi yake kwake ya kumuunga mkono jitihada zake

Katika hatua nyingine Msanii huyo wa kuchora picha amemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabil Omary Makame kwa msaada mkubwa alioutoa  kwa kumsaidia kumfikia Mkuu wa Mkoa ambaye nae kwa dhamira yake njema kumzawadia shilingi milioni moja          (Tsh. 1,000,000.00) huku akitoa wito kwa watanzania wote kumuunga Mkono Rais katika kampeni hiyo.

“ninaomba kwamba, hii picha imfikie mwenyewe mhusika Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ili aweze kutiwa moyo kwa kampeni aliyoianzisha na wote tuweze kujitahidi kumuunga Mkono tuweze kufikia mafanikio makubwa zaidi” amesema Msanii Mboya Hosiana.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabil Omary Makame (kushoto kabisa) akishuhudia tukio muhimu la Mkuu wa Mkoa kupokea zawadi ya Rais 

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.