• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC SHIGELA APONGEZA WANAKIKUNDI CHA JAMII MPYA KUFANYA UTALII WA NDANI.

Posted on: May 14th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amewapongeza Wanakikundi cha Jamii Mpya Tanzania kwa uamizi wao wa kufanya Utalii wa ndani Katika Mbuga ya wanyama ya Mikumi ishara ya kuunga mkono jitihada za Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutangaza Vivutio vya Utalii wa nchi kupitia Filamu ya Royal Tour.



Martine Shigela ametoa pongezi hizo leo Mei 14 wakati wa ziara yake ya kuwatembelea Watanzania zaidi ya 1000 kutoka Mikoa mitatu ya Morogoro, Pwani na Dar es Salaam waliotembelea Mbuga ya Mikumi kama sehemu ya kutoa hamasa kwa wananchi wengine kuweza kufanya utalii wa ndani ili kuchangia pato la taifa na kukuza uchumi wa taifa.



Aidha, Martine Shigela amebainisha kuwa, kuamua kuunga mkono jitihada za Rais kwa vitendo kutatoa sura mpya kwa vijana na wananchi wa Tanzania kwa ujumla kujiajili na kuweza kuendesha Maisha kwa kujipatia kipato kwa kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi na kimaendeleo hasa kwa jamii iliyo karibu na maeneo husika ya Utalii.





“Wapo Tourguide hapa wanaojitolea na wamesomea ambao hawaajiliwi na Serikali lakini wanaijua sana Mbuga na wananaweza kukuelekeza vizuri, ukitaka kumuona simba twende huku.." amesema Shigela.

"akinamama wanaozalisha mbogamboga, mayai, maziwa, matunda na kuku watapata masoko kwa sababu wageni wakija watahitaji chakula” ameongeza Martine Shigela.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amesema biashara yoyote ili iwe na mafanikio ya haraka na ya kweli lazima yawe na matangazo kama ambavyo Mhe. Rasi Samia amefanya kitaifa na kimataifa katika kuitangaza Filamu ya Royal Tour.





Naye Naibu Kamishina wa Uhifadhi kanda ya Mashariki Bi Asteria Ndaga amewapongeza vijana hao kwa kuwa vijana wa kihistoria, kwani tangu kuanzishwa kwa utalii Katika taifa hili vijana hao ndio waliotalii kwa idadi kubwa na kwa mara moja.




Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Mikumi Mhe. Dennis Londo ameweka wazi kuwa kitendo hicho walichofanya vijana hao kitaitangaza Mbuga hiyo ya Mikumi na kusaidia kuleta watalii wengi zaidi kutoka ndani na nje ya nchi hivyo kuleta mafanikio makubwa katika taifa kupitia sekta ya utalii.




Zaidi mwenyekiti wa Kikundi cha Jamii Mpya Tanzania Bi. Magdalena Nachunga amesema kwa kuanzia wameanza kutalii Mbuga hiyo ya Mikumi lakini lengo kuu si kuishia hapo bali ni kuzunguka na kutoa hamasa nchini nzima lengo ni kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili utalii uweze kuwanufaisha watanzania wote kikamilifu.






MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.