• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC SHIGELA ATAKA JITIHADA KUTOKOMEZA MIMBA ZA UTOTONI.

Posted on: May 10th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela ameziagiza Taasisi za Serikali, Mashirika binafsi pamoja na Taasisi za kidini kushirikiana na kuongeza jitihada za kutokomeza mimba za utotoni Mkoani humo kwa Watoto walio chini ya miaka 21 kwa wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari.

 



Martine Shigela ametoa agizo hilo Mei 10 Mwaka huu wakati akifungua Mkutano wa kutambulisha Mradi wa Kutokomeza Mimba za Utotoni unaotarajia kuendeshwa na tasisi ya RELIEF TO COMMUNITY DEVELOPMENT ORGANISATION ( RECODO) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo na kushirikisha wadau mbalimbali.


 




Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa lazima uwepo ushirikiano baina ya taasisi za kidini, taasisi za Kiserikali, Mashiririka binafsi pamoja wadau wengine wakiwemo wazee wa kimila katika kuhakikisha changamoto ya mimba za utotoni inatokomezwa kabisa Mkoani humo, kwani suala la kupunguza au kutokomeza mimba utotoni ni suala jumuishi na sio suala la Taasisi moja.

“hili si jambo la Recodo peke yao bali ni jambo la  jamii kwa ujumla na ndio maana tukashirikisha taasisi nyingi wakiwemo viongozi wetu wa dini ili sasa kuja na paper itakayotuongoza nini kifanyike, nani afanye nini kwa wakati gani. Nadhani tukija na hio paper itatusaidia kuwa na wider platform itakayohusisha viongozi wa Wilaya lakini pia Viongozi mbalimbali watakao kuja kushiriki Kikao chetu”. amesema Martine Shigela.





Katika hatua nyingine, Martine Shigela ameongeza kuwa ili kuhakikisha mtoto wa kike anasaidiwa kufikia malengo yake,a Serikali ya awamu ya sita chini ya Uongozi wa Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tayari imetenga fedha kwa kila jimbo Mkoani humo kwaajili ya kujenga Shule za Sekondari Mahsusi kwa ajili ya kuwasaidia Watoto wa kike ili kutimiza ndoto na malengo yao na sio kukatishwa malengo kwa sababu ya changamoto ya mimba za utotoni.






Kwa upande wake Mkurugenzi wa taasisi ya RECODO Bwana Saidi Muya ameeleza kuwa kama taasisi wanapokea na kufanyia kazi maagizo ya Mkuu wa Mkoa na kwamba watatanua wigo kwa kushirikiana na wadau wengine sio tu kwa kutokomeza mimba za utotoni bali watapambana pia na masuala ya mapenzi ya jinsia moja kwani nayo ni sababu ya Watoto kuharibika na kuachana na masomo bila kutarajia.






Akiwakilisha vyombo vya ulinzi na usalama Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi Fortunatus Muslim amesema kwamba ili RECODO waweze kufanikisha shughuli hiyo ni lazima wapate uzoefu wa ukusanyaji wa data kutoka kwa wadau wazoefu likiwemo Jeshi la Polisi kupitia kitengo cha dawati la jinsia kwa lengo la kukomesha kabisa masuala ya ubakaji, mimba za utoto na ulawiti hali itakayowezesha Watoto na wanafunzi kutimiza malengo na ndoto zao za kupata Elimu.


 






MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.