• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Shigela ataka Morogoro isiyo na Migogoro.

Posted on: June 22nd, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amedhamiria kuufanya Mkoa wa Morogoro kuwa ni Mkoa usio na Migogoro na kuondoa dhana iliyojengeka miongoni mwa Watanaznia wengi kuwa Mkoa huo ni Mkoa wa mapigano, vurugu na migogoro baina ya wakulima na wafugaji jambo ambalo amesema kwa sasa linaanza kuwa ni historia.

Shigela ametoa kauli hiyo Juni 21, mwaka huu wakati wa hafla fupi ya uwaapisho wa Wakuu wa Wilaya watano walioteuliwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hafla iliyofanyika katika viwanja vya Ikulu ndogo Mjini Morogoro huku akiwataka Wakuu hao wa Wilaya kuubrandi Mkoa huo kuwa na TASWIRA nzuri.

RC Martine Shigela akiwa na  RAS Bi. Mariam Mtunguja mara baada ya kuapishwa kwa Wakuu wa Wilaya wa Mkoa wa Morogoro.

Shigella amesema Mkoa wa Morogoro ni Mkoa mzuri, una rasilimali nyingi ambazo ni nadra kuzipata katika Mikoa mingine ya nchi hii ikiwa ni pamoja na kuwa na zaidi ya mito mia moja inayotiririsha maji kwa mwaka mzima.

DC Mvomero Halima Okash akisikiliza maelekezo ya RC Shigela.

Rasilimali nyingine alizozitaja zilizopo ndani ya Mkoa huo ni pamoja na uwepo wa maeneo makubwa ya Ardhi, Ardhi  yenye rutuba, hali ya hewa safi, pamoja na vivutio mbalimbali vya Utalii ikiwemo maporomoka ya Maji na wanyama pori.

Vingine ni hifadha za misitu, hifadhi ya mazingira asili ambapo vinapatikana vinyonga aina yake wenye pembe tatu wanaopatikana katika milima ya Uluguru, na wanyama aina ya sheshe na panzi wenye rangi ya Bendera ya Taifa letu ambao wote wanapatikana katika bonde la Mto Kilombero pekee. Pia kuna misitu na mbuga za wanyama kama Mikumi, Udzungwa  na Hifadhi ya Taifa ya  Nyerere.

Pamoja na kuzitaja rasilimali na vivutio hivyo kwa uchache, Shigela amesema Mkoa wa Morogoro umekaa kimkakati zaidi kiuchumi katika maana ya upo katikati kimawasiliano ambapo unapitiwa na Reli ya Kati, Reli ya TAZARA, na sasa inajengwa Reli ya Mwendo Kasi – SGR ambayo nayo inakatisha katikati ya Mji wa Morogoro.

Amesema Mkoa huo pia unapitiwa na Barabara kuu iendayo mikoa yote ya nyanda za juu kusini mwa nchi yetu na Mikoa mingi iliyoko kanda ya kati na ile iliyopo Kaskazini mwa nchi hii na nchi nyingine jirani.

Kutokana na uzuri wa rasilimali na fursa hizo, Mhe. shigela amesema kuna haja sana ya kuutangaza Mkoa wa Morogoro na kuyatangaza mazuri hayo yaliyopo ili kufuta dhana ya Watanzania wengi ambao wamezoea kusikia vurugi pekee zinazojitokeza Mkoani humo badala yake wayaone mazuri mengi ambayo yamefichwa na hayo mabaya machache.

 ‘’Tunayo mengi mazuri tu ya kufanya, tuubrand Mkoa, duniani kote wanabrand mambo mazuri. Hata kama kuna mengine mabaya unasema ili tuangalie namna ya kurekebisha’’ amesema Shigella.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa ametoa wito kwa waandishi wa  Habari wanaowakilishi vyombo vyao vya habari Mkoani humo kutoa ushirikiano katika kuutangaza Mkoa huo na kutangaza mambo mema yanayofanyika na yaliyopo ndani ya Mkoa huo huku akiwapongezi kwa kazi nzuri wanazozifanya.

“Tunawajibu wa kuibrandi picha ya morogoro kuwa nzuri, brand yetu siyo nzuri, brand ya Mkoa wa Morogoro ni vurugu, migogoro na ugomvi, ukiona tangazo la Morogoro kwenye TV utegemee mabaya, sasa na nyie waandishi wa habari mpunguze hayo, duniani kote wanabrandi vizuri tu” amesema Shigela.

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.