• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Shigela ataka somo la lishe lifundishwe Shuleni.

Posted on: July 16th, 2021

 
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amewataka  Maafisa Elimu Mkoani humo kuweka mpango mkakati wa somo la lishe kufundishwa shuleni   ili  kutokomeza  utapiamlo kwa watoto walio chini ya miaka mitano.

Shigela ametoa agizo hilo  Julai 16 mwaka huu kwenye kikao cha nusu mwaka kilicholenga kutathimini Mkataba wa mpango wa lishe na Bima ya Afya ya jamii iliyoboreshwa yaani iCHFkilichifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Gronency katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Shigela amesema, kufundishwa kwa somo hilo Shuleni kutawasaidia wanafunzi kutambua matumizi Bora na sahihi ya vyakula ambavyo vinatakiwa kuliwa kwa kuzingatia kanuni na miongozo inayotolewa na wataalam wa Afya hivyo kuwajengea Afya nzuri watoto hao.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa huyo amewaagiza Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri zote za Mkoa wa Morogoro  wakishirikiana na Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri wa Mkoa huo kuendelea kuweka jitihada za kutafuta mbinu mbalimbali za kuongeza idadi ya wanachama wa Mfuko wa Bima ya Afya iliyoboreshwa (iCHF).

Sambamba na hilo Shigela amewataka viongozi hao zoezi la kuongeza wanachama liende sambamba na uboreshaji wa huduma za Afya kwa wanachama wake ili wanachama hao waone umaana wa Kujiunga na Mfuko huo na kuondoa malalamiko yanayotolewa na wanachama wake katika maeneo yetu ya kutolea huduma ya Afya kuwa hawapata dawa kupitia Bima hiyo.

‘’Bado Mkoa wetu wa Morogoro tuna changamoto kubwa ya Bima hii ya Afya iliyoboreshwa, asilimia ya wanachama wetu tuliowaandikisha hawapati huduma kama inavyostahili, kumekuwa na malalamiko sana katika upande huu wa Bima, wengi wanalalamika kuwa dawa hakuna wakati sehemu zingine dawa zipo’’ amesema Shigela.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa huo Bi. Mariam Mtunguja amebainisha moja ya changamoto inayokabili Bima ya Mfuko wa iCHF ni kutokuwepo wanachama wa kudumu kutokana na huduma zisizo aminika ambazo hupelekea wanachama hao kutohuhisha bima zao mara tu baada ya kuisha muda wake.

Hata hivyo, Bi. Mtunguja amewataka Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Halmshauri zote za Mkoa huo kuwa mstari wa mbele katika kutoa Elimu juu ya faida mbalimbali ambazo zinatokana na (iCHF) ili kuongeza idadi ya wanachama wa kudumu katika mfuko huo.

Awali akiwasilisha taarifa ya Mfuko wa Bima ya Afya Mratibu wa CHF Mkoa wa Mrogoro Bi. Elicia Mtesigwa amesema bado wanaendelea na uhamasishaji ili kuyafikia makundi mbalimbali ndani ya jamii ili yajiunge na mfuko,  huku akieleza lengo lake sio tu kuwa na wanachma wengi bali kuhakikisha kila mwananchi Mkoani humo anakuwa na uhakika wa kupata matibabu ya Afya wakati wote hata anapokuwa hana fedha mkononi.

Pia, Bi. Elicia amebainisha kuwa zaidi ya wanachama 56, 000 Mkoani Morogoro wamejiandikisha katika mfuko wa Bima ya Afya iliyoboreshwa kwa mwaka wa fedha 2020/2021 sawa na asilimia 9.5 ya kaya 590,006 ambapo kaya 21, 941 kati ya hizo zinaweza kupata matibabu katika vituo vya kutolea huduma za Afya.

Mpango wa Bima ya Afya ya iCHF ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi  CCM ndicho kilichounda Serikali iliyopo madarakani, ambapo katika Ibara ya 83 (e) ukurasa wa 186 inazungumzia uimarishaji wa  mifuko ya Bima ya Afya nchini ikiwemo  NHIF na CHF) ili kufikia lengo la Serikali la kuwa na Bima ya Afya kwa wananchi wote hapa nchini.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.