• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Shigela atoa leseni ya Uchimbaji wa madini na kuisimamisha

Posted on: May 28th, 2022

RC shigela asitisha leseni, muda mfupi baada ya kuitoa

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amesitisha leseni ya uchimbaji na ununuzi wa madini muda mfupi baada ya kuitoa kwa kikundi kimoja cha uchimbaji madini ya dhahabu katika kijiji cha Kitaita Wilayani Gairo Mkoani humo baada ya kunusa uwepo wa dhuluma wanaoweza kufanyiwa wachimbaji wadogo wa madini wa eneo hilo.

 Martine Shigela amefikia uamuzi huo Mei 26 mwaka huu alipofanya ziara ya kawaida ya kukagua miradi ya maendeleo na kutatua kero za wananchi Wilayani Gairo ambapo alifika pia katika Mgodi wa Madini ulioko katika Kijiji cha Kitaita ili kujionea namna shughuli za uchimbaji wa madini wa eneo hilo unavoendelea.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akiongea na wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu (hawapo pichani) katika kijiji cha Kitaita Wilayani Gairo

Katika eneo hilo Mkuu huyo wa Mkoa alipokea changamoto mbalimbali za wachimbaji hao ikiwemo bei ndogo ya ununuzi wa madini pamoja na utata wa asilimia ya viroba vya mchanga wenye madini vinavyotakiwa kuchukuliwa na Kikundi cha madini cha Nguvu moja ambacho kiliomba kumilikishwa sehemu ya ardhi ya mgodi huo wa dhahabu ambacho tayari kilikuwa kimekupewa leseni hiyo na kiongozi huyo muda mfupi baada ya kufika.


Mwenyekiti wa Chama (CCM) Wilaya ya Gairo Shaban Sajilo akiongea na wachimbaji wadogo wa madini 

Baadhi ya Viroba vya mchanga wa dhahabu vinavoonekana hapo

RC Shigela akikagua eneo la uchimbaji madini, kushoto kwake ni Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa huo Mhandisi Ezron Kilamhama

Hii ndo hali halisi ya machimboni

Baada ya Mkuu wa Mkoa kupokea changamoto hiyo na wahusika akiwemo Afisa Madini Wilaya ya Gairo Tito Mahela kushindwa kutoa kwa kina ufafanuzi wa changamoto hiyo, Martine Shigela akalazimika kusitisha matumizi ya leseni aliyokuwa ameitoa muda mfupi kwa kikundi cha nguvu kazi na kwamba uchimbaji huo uendelee kufanyika kama ilivyokuwa awali kabla ya leseni hiyo lutolewa hadi Juni 4 mwaka huu atakapokutana na pande zote zinazohusika akiwemo Afisa Madini Mkoa wa Morogoro ili kulipatia ufumbuzi suala hilo.

 “…..suala la mgawanyo baina ya mwenye Leseni na yule asiye na Leseni, jambo hilo nalisitisha mpaka wakalieleze vizuri ofisini” amesema Shigela.

“Tarehe 4 asubuhi nitakuja Gairo hapa, nitakuja na Afisa madini wa Mkoa, chagueni wawakilishi kumi baina ya wanunuzi na wachimbaji wadogo na hii Leseni isimame kwanza hadi tutakapoafikiana juu ya utaratibu wa hapa” amesisitiza Shigela.

Pamoja na kusitisha leseni hiyo na kuwataka watu wachimbaji kuendelea na utaratibu wa awali wa kuchimba madini Shigela amewataka wachimbaji hao kufanya biashara hiyo kwa kufuata miongozo yote ya kiserikali ili Serikali nayo iweze kupata mapato yake.



RC Shigela akitoa leseni ya umiliki wa sehemu ya eneo la uchimbaji madini muda mfupi kabla hajasimamisha matumizi ya leseni hiyo

Onyo la RC Shigela kwa wachimbaji na wafanya biashara wa madini 

“Ni kinyume cha Sheria na ni kosa kubwa sana kuiba madini, kutorosha madini na kwenda kuuza katika utaratibu usiokubalika katika nchi yetu”. Ameonya Shigela.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabiri Omary Makame pamoja na kuwapongeza wachimbaji madini kwa kushiriki kutoa tozo na ushuru wa aina mablimbali kupitia madini hayo, amemuomba Mkuu wa Mkoa kuingilia kati suala la changamoto za miundombinu ya barabara na ukosefu wa maji safi na salama suala ambalo Mkuu wa Mkoa  amemuagiza Meneja wa TARURA na Meneja wa RUWASA Wilayani humo kushughulikia kero hizo mara moja.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabil Makame (katikati) akishuhudia RC akitoa leseni ya umiliki wa eneo la uchimbaji wa madini

Kamishina Msaidizi mwandamizi wa Polisi Fortunatus Musilimu ambaye ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro amewahakikishia wachimbaji wa madini wa Kitaita ulinzi imara katika eneo la mgodi huku akiwaomba kutoa ushirikiano wao kwa jeshi la Polisi kwa kuwa watu katika eneo hilo ni wengi hivyo unatakiwa ushirikiano wa dhati na kulazimika Kamanda huyo kutoa namba yake simu ya kiganjani kwa ajili ya mawasiliano zaidi.

Afisa Madini Wilaya ya Gairo Tito Mahela amefafanua suala la bei ya uuzaji wa madini kuwa bei elekezi ya kununua madini katika eneo la uchimbaji ni shilingi 100,000/= hata hivyo  yule asiyeridhika na bei hiyo afuate utaratibu wa kupata kibali ofisini kwake ili kwenda kuuza madini yake katika soko ambalo lipo Kisheria Wilayani Gairo ambapo dhahabu itanunuliwa kwa shilingi 123,000/=

Afisa Madini Wilaya ya Gairo Titus Mahela (katikati)

Aidha wachimbaji wa madini baada ya kusikilizwa kero zao ambazo zilipewa majibu sahihi, wameiomba Serikali isiwasahau kwenye zoezi la sense ya watu na makazi linalotarajiwa kufanyika Agosti 23 mwaka huu, kwa kuwa wamesema muda huo wao watakuwepo eneo la machimbo kwa kuwa hizo ndio shughulia zao za kila siku lakini wanaomba kuhesabiwa.



Umati wa wachimbaji wa madini eneo la Kitaita waliokusanyika kutoa kero zao kwa Mkuu wa MKoa

 

 MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.