• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Shigela atoa Viwanja kwa Wachezaji wa Mtibwa.

Posted on: June 22nd, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro  Martine Shigela amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Morogoro  Albert Msando na Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Pascal Kihanga  kutenga eneo lenye hekari 4,500 kwaajili ya kuwagawia viwanja vijana wa timu ya Mtibwa Suger wenye umri chini ya miaka 20 walioshiriki michuano ya ligi ya vijana mwaka huu.

Shigela ametoa agizo hilo Juni 22, mwaka huu wakati wa hafla ya kuwapokea mabingwa hao wakitokea Dar es Salaam hafla iliyofanyika Bwalo la Umwema katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro baada ya vijana hao kuibuka mabingwa wa mashindano hayo mara tatu mfurulizo katika michuano ya ligi ya vijana chini ya umri huo.

Mkuu wa Mkoa Martine Shigela ametoa ametoa agizo la vijana hao kupewa viwanja ili kuwaenzi wachezaji hao, na kwa kufanya hivyo watakuwa wametoa hamasa kwao na kuthamini mchango wao katika tasnia ya michezo.

 ‘’..watengeneze mtaa kuenzi timu hii katika Mkoa wetu na Manispaa yetu tunauita MTAA WA MTIBWA SUGER AU MTIBWA SPORTS halafu wanajenga nyumba zao pale, sasa mstahiki meya nadhani umenielewa na DC, mkubwa huwa haombi anaongea kidiplomasia lakini ameagiza hivyo…’’ amesema Shigela.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Halima Okash amewatia moyo mabingwa hao akiwaeleza umuhimu wa michezo ambapo amesema mpira ni Afya, mpira ni ajira lakini pia mpira unawasaidia kutambulika kitaifa na kimataifa kwa kujuana na watu mbalimbali katika sekta ya michezo.

Sambamba na hayo, Mkuu huyo wa Wilaya amesema ameahidi kuwa bega kwa bega na  timu hiyo katika kuiunga mkono na kuitangaza ili iweze kufika pale ambapo inatarajia.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoani humo (MRFA) Pascal Kihanga ametoa wito kwa viongozi wa timu ya Mtibwa suger kutowazuia wachezaji hao vijana kusajiliwa na timu nyingine pale wanapohitaji kusajiliwa kwa kuwa hiyo ndiyo ajira yao.

Hata hivyo Pascal Kihanga ametahadharisha kuwa jambo hilo pamoja na kuwa litaleta sifa ndani ya Mkoa wa Morogoro na timu ya Mtibwa suger kwa kuonekana kuwa ni kiwanda cha kuzalisha wachezaji lakini litafutiwe utaratibu unaofaa katika maana ya kuwa na mikataba yenye kuleta faida kwa pande zote tatu yaani club inayouza, inayonunua na kwa mchazaji mwenyewe.

Mkurugenzi wa Mtibwa Ndg. Abel Magesa amesema wachezaji hao huchukuliwa wakiwa wadogo kutoka maeneo mbalimbali ambapo wanalelewa na kutunzwa kwa gharama kubwa  wakiwa na imani ya kupata wachezaji wazuri hapo baadae ambao mara nyingi husajiliwa na kuchezea timu kubwa za hapa nchini zikiwemo timu ya Yanga na Simba.

‘’Tumekuwa  kisima cha kutoa wachezaji mashuguri kwenye vilabu vya Simba na Yanga na hata timu nyingine mashuhuri, kwa sababu wanajua Mtibwa Suger ni kina cha kuchota maji kwa ajili ya kandanda’’ amesema Magesa.

Awali akizungumza katika  hafla hiyo, msemaji wa timu ya Mtibwa Suger Thobias Kifaru ameeleza kuwa timu yao ni chuo cha kuandaa wachezaji wa mpira wa miguu, huku wachezaji wa kikosi hicho akiwemo Abdul Kapirima na Frank George wametoa pongezi zao kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kwa mapokezi mazuri ambayo hayakuwahi kutokea  na kuahidi kuongeza juhudi ili kuendelea kuchukua ubingwa kwa mashindano yajayo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.