• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Shigela awatoa hofu wanamorogoro chanjo ya COVID - 19

Posted on: August 30th, 2021

RC Shigela awatoa hofu Wanamorogoro kuhusu chanjo ya UVIKO – 19.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amewatoa hofu wakazi wa Mkoa huo na watanzania wote kwa ujumla kuhusu chanjo ya UVIKO – 19 huku akieleza kuwa chanjo hiyo ni salama na inalenga kuokoa maisha ya watanzania na si vinginevyo.

Baadhi ya wajumbe wa kikao hicho wakiwa kwenye kikao

Shigela ametoa rai hiyo wakati akifungua kikao cha uhamasishaji wa chanjo ya UVIKO – 19 kwa wawakilishi wa Taasisi mbalimbali zilizopo Mkoani humo zikiwemo taasisi za kidini kwa lengo la kupata elimu ya chanjo hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

Wajumbe kutoka taasisi mbalimbali walioshiriki kikao hicho

Amesema, propaganda zinazotolewa na baadhi ya mitandao ya kijamii kutoka kwa baadhi ya watanzania sio za kweli na zinalenga kudhoofisha Afya za Watanzania na juhudi za Serikali za kupambana na ugonjwa wa UVIKO – 19.

“yamekuwepo maneno hasa kwenye sekta hii ya chanjo dhidi ya CORONA kulingana na tafasiri mbalimbali za watu… wakiwa na nia ileile ya kutaka kudhoofisha Afya za Watanzania lakini pia kurudisha nyuma jitihada za Serikali ya Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan za kupambana na ugonjwa wa CORONA” alisema Martine Shigela.

wakati wa Kikao wajumbe walipewa Elimu ya chanjo ya UVIKO - 19

Katika hatua nyingine, Shigela amewataka viongozi wenzake kusimamia suala hilo kwa umakini huku akiwatoa hofu kuwa chanjo hiyo ni salama na ina nia njema na watanzania na kubainisha kuwa yeye ndiye mtu wa kwanza kupata chanjo ya UVIKO – 19 katika Mkoa wa Morogoro hivyo watu wasiwe na hofu bali kila mmoja kwa hiari yake achukue jukumu la kwenda kuchanja.

Taasisi za Serikali na Vyamba vya siasa pia walishiriki kikao hicho

Mratibu wa UKIMWI Mkoa wa Morogoro ambaye pia ndiye mratibu wa Chanjo ya UVIKO – 19 Mkoa wa Morogoro Dkt. Masumbuko Igembya ameeleza lengo la kikao hicho kuwa ni kuendelea kuweka mikakati madhubuti ya zoezi hilo la chanjo ili watu waepukane na ugonjwa wa UVIKO – 19.

Aidha, Dkt. Masumbuko amesema faida Msingi na kubwa ya chanjo ya UVIKO - 19 ni kupunguza madhara makubwa ya ugonjwa huo iwapo mtu ataambukizwa chanjo itamsaidia aindelea kuwa salama.

Mratibu wa Chanjo Mkoa wa Morogoro Dkt. Masumbuko Igembya akisikiliza kwa makini maswali ya wajumbe ili ayatolee ufafanuzi

Kwa upande wao washiriki wa kikao hicho akiwemo Askofu Jacob Mameo wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania - KKKT Dayosisi ya Mashariki amewataka watanzania wasidanganyike na maneno ya kwenye mitandao kwamba chanjo hiyo sio salama, kwani amesema hakuna kiongozi wa Serikali Duniani anayeweza kudiliki kudhuru watu wake huku akishuhudia kuwa yeye pia amechanjwa chanjo hiyo na afya yake iko vizuri.

Viongozi kutoka Taasisi za kidini wakisikiliza kwa makini Elimu ya Chanjo ya Uviko - 19

Katibu wa Baraza la Wazee Mkoa wa Morogoro Bakili Anga, yeye amekwenda mbali zaidi kuwa pamoja na chanjo hiyo ina malengo ya kupambana na ugonjwa wa CORONA bado ina faida zaidi kwani kabla ya kuchanja chanjo ya COVID – 19 alikuwa anasumbuliwa na homa ya malaria kila baada ya miezi sita lakini mara baada ya kuchanjwa hajapata homa hiyo ya malaria.

Naye katibu wa BAKWATA Mkoa wa Morogorom Ahmad Khairalah ameeleza kuwa kutokana na elimu aliyoipata katika kikao hicho amewataka watanzania wajitokeze kwa wingi  kupata chanjo ili wajikinge na afya zao ikiwa ni kwa manufaa yao na wengine.

Kwa mujibu wa Dkt. Masumbuko Igembya, Halmashauri ya manispaa ya Morogoro inaongoza kwa wananchi wake kuhamasika kwa kupata chanjo kwani hadi sasa watu 5,051 wamechanjwa sawa na asilimia 72 ya wananchi wanaotakiwa kuchanjwa katika Halmashauri hiyo.


MWISHO.

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.