• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

REA MKOANI MOROGORO KUMCHUKULIA HATUA MKANDARASI WA KAMPUNI YA HXJDL.

Posted on: January 26th, 2023

Bodi ya Wakala ya Nishati ya umeme Vijijini (REA) imepanga kumchukulia hatua kwa kumsimamisha kazi Mkandarasi wa Kampuni ya HNXJDL kutoka nchini China kwa kushindwa kukamilisha mradi wa kuunganisha umeme katika Vijiji 146 Mkoani humo Morogoro.

Kauli hiyo imetolewa Januari 26 mwaka huu na Bwana Styden Rwebangila Mjumbe wa Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) baada ya kikao kilichowakutanisha wadau wa nishati Mkoani  Morogoro wakiwemo Wabunge wa Mkoa huo kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Mjumbe wa Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Styden Rwebangila, akizungumza na waandishi wa habari baada ya kikao.

Bwana Rwebangila amesema Mkandarasi huyo alipewa tenda ya kukamilisha mradi wa kuunganisha umeme katika Vijiji 146 ambapo Vijiji 36 pekee amekamilisha huku muda wa kukabidhi mradi huo ni Februari 18, 2023.

Aidha, baada ya majadiliano na wajumbe wa kikao hicho wameazimia kumpunguzia maeneo ya mradi huo kwa kuyagawa kwa wakandarasi wengine na kumtaka Mkandarasi huyo kukamilisha mradi huo kwa wakati katika maeneo machache aliyobaki nayo.

“...kumpunguzia kazi angalau asilimia 50 ili aweze kubaki na Vijiji vichache na wananchi wapate umeme kama Serikali ilivyo kusudia”. amesema Bwana Rwebangila.

Sambamba na hilo Bwana Rwebangila amesema Serikali imeamua kuongeza vigezo kwenye utoaji wa tenda kwa wakandarasi kwa lengo la kuwapata wakandarasi wenye sifa na uzoefu wa kukamilisha miradi yao kwa wakati.

Kwa upande wake Mbuge wa Mikumi na Katibu wa Wabunge Mkoa wa Morogoro Mhe. Denis Londo amesema kwa muda mrefu wananchi katika Jimbo lake wanamlalamikia kwa kushindwa kutekeleza ahadi yake aliyoitoa wakati wa kampeni za uchaguzi ya kuhakikisha kuwa kila kijiji ndani ya Jimbo hilo kinapata huduma ya umeme.

Mhe. Denis Londo Mbunge wa Mikumi akielezea kutokufurahishwa na kasi ya Mkandarasi ya kutekeleza Miradi ya umeme katika Jimbo lake.

Aidha, Mhe. Londo amesema hawakubaliani na kasi ya  Mkandarasi huyo katika kutekeleza kazi yake ndani ya Jimbo hilo hivyo kupitia kikao hicho wamekubaliana kumpunguzia maeneo ya mradi huo kutokana na kuchukua maeneo mengi na kushindwa kukamilisha kazi kwa wakati kama mkataba unavyoelekeza.

Nae Mbunge wa Malinyi Mhe. Antipas Mgungusi ameishukuru Serikali kwa kuunganisha umeme katika Jimbo lake ambapo kati ya Vijiji 33, Vijiji 32 vimeshaunganishwa na umeme kwa awamu ya kwanza na wanatarajia mradi wa Ujazilizi ambapo vitongoji vyote ndani ya Wilaya hiyo vitaunganishwa na huduma ya umeme.

Mradi huo wa kuunganisha umeme awamu ya tatu katika Mkoa huo ulikuwa unatekelezwa na Wakandarasi wawili ambapo Mkandarasi wa Kampuni ya STEG tayari imekamilisha miradi yake kwenye Vijiji 83 katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro.

Miradi hiyo ya kuunganisha umeme Mkoani Morogoro unagharimu kiasi cha shilingi Bilioni 71.




MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.