• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RUWASA NENDENI MKALITENDEE HAKI HILI GARI - RC MALIMA.

Posted on: October 24th, 2024



Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima ameitaka Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) kulitumia vyema gari jipya katika kuyafikia maeneo yote ya miradi ya maji ambayo hapo awali yalikuwa hayafikiki kutokana na upungufu wa magari katika mamlaka hiyo ya Wilaya ya Malinyi.

Mhe. Malima amebainisha hayo Oktoba 24, Mwaka huu wakati wa tukio la kukabidhi gari jipya kwa RUWASA lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu huyo wa Mkoa.

Aidha, Mhe. Adam amesema lengo kubwa la kukabidhi gari hilo Wilayani humo ni kutokana na upungufu wa magari kwa RUWASA  kushindwa kufika kukagua miradi ya maji inayotekelezwa Wilayani humo, hivyo ameitaka mamlaka hiyo kwenda kufanya kazi kwa bidii na kulitumia gari hilo kwa lengo kuwaondolea wananchi adha ya maji.

".. watu wa idara ya maji, Mkurugenzi na viongozi wengine mkalitendee haki kwa matumizi ya gari hili kuweza kuifikia miradi na maeneo yote ya Malinyi na kutatua changamoto za maji..." Amesisitiza Mhe. Adam Malima


Pia Mkuu huyo wa Mkoa amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan  kwa kuwatazama Wananchi wa Wilaya ya Malinyi Mkoa wa Morogoro kwa kuwaletea gari kwa ajili ya RUWASA ili kuwatumikia wananchi hasa kutatua changamoto za maji.


Kwa upande wake, Mhandisi Sospeter Lutonja Meneja wa RUWASA wa Mkoa wa Morogoro amesema kupitia Serikali ya awamu ya sita  inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mkoa huo umeendelea kupokea fedha za miradi ya maji ambapo kwa sasa  miradi 64 inaendelea yenye thamani ya shilingi Bilioni 89.


Ameendelea kwa kusema moja ya changamoto wanayoipata watendaji wa RUWASA waliopo ngazi za Wilaya ni upungufu wa magari ambapo inawapelekea kushindwa kufika katika miradi ya maji hivyo amemshukuru Mhe. Rais kwa kuwaona Wananchi wa Malinyi na kuweza kutoa gari ambapo itaenda kuondoa changamoto za maji kwa wananchi.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.