• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

"SAMIA KILIMO BIASHARA EXPO 2024" KULETA MAGEUZI YA KILIMO, UFUGAJI MOROGORO

Posted on: September 15th, 2024

Maonesho ya Kilimo Biashara na Mikutano ya Wakulima na Wafugaji (SAMIA KILIMO BIASHARA EXPO 2024) yamelenga kuleta mageuzi katika sekta ya Kilimo, ufugaji na mazingira ili kuongeza tija na uzalishaji katika sekta ya kilimo na mifugo.

Hayo yamebainishwa Septemba 15, Mwaka huu na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima wakati akiongea na waandishi wa Habari katika ukumbi wa mikutano wa ofisi yake kuhusu Maonesho ya Kilimo Biashara yanayoitwa “SAMIA KILIMO BIASHARA EXPO 2024, MSIMU WA 3” yanayotarajiwa kufanyika Wilayani Gairo kuanzia Oktoba 6 - 12, 2024 yakiwa na lengo la kuwasaidia wakulima na wafugaji kupata huduma na kujifunza teknolojia na mbinu bora za uzalishaji.

Akifafanua zaidi, Mhe. Malima amesema maonesho hayo pia yamelenga kutekeleza maono ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo na ufugaji kupitia mkakati wa Ajenda 10/30 ambao unalenga kuongeza kasi ya ukuaji wa sekta ya kilimo kufika 10% ifikapo mwaka 2030 kutoka asilimia 4.2% Mwaka 2023.

“…tunatakiwa kulima kiteknolojia kwa kutumia nguvu na mtaji kidogo kupata kipato kikubwa ili kupata chakula cha ziada na kuweza kuondoa umasikini…” amesema Mhe. Adam Kighoma Malima

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amesema dira na mikakati ya Mkoa kwa Wilaya ya Gairo, ni kuwasaidia wananchi kulima na kufuga kwa tija kupitia mazao ya asili yanayolimwa Wilayani humo sambamba na mazao mbadala ya kimkakati kama parachichi, viazi mviringo na tumbaku, ikiwa ni nyenzo muhimu ya kukuza vipato vya wananchi wa Wilaya hiyo.

Kwa muktadha huo, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wananchi kuendelea kujikita katika kilimo mazao, kilimo uvuvi na kilimo mifugo sambamba na utunzaji na uhifadhi wa mazingira kwa kutumia nishati safi ya kupikia ikiwemo gesi, umeme, mkaa mweupe na njia nyingine mbadala ili kutunza vyanzo vya maji ambavyo vinachochea kupata mazao bora.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Jabir Makame amesema, zaidi ya asilimia 95 ya wananchi wa Wilaya hiyo wanajishughulisha na sekta ya kilimo pamoja na mifugo hivyo maonesho hayo ya Kilimo biashara ni muhimu katika kutoa mafunzo ya kutumia teknolojia ya kilimo kwa uzalishaji wenye tija.

Kwa sababu hiyo, Mhe. Makame amesema Wilaya hiyo imeamua kuchukua hatua madhubuti ya kukabiliana na changamoto zinazoikumba sekta ya kilimo na mifugo ikiwemo tija ndogo na kufanya maonesho ili kuwakutanisha wadau wote wanaohusika katika mnyororo wa thamani wa sekta ya kilimo, mifugo na mazingira.

Amebainisha wadau wanaohitajika kukutana katika msimu huu wa tatu wa maonesho hayo kuwa ni pamoja na waukima na wafugaji, wauzaji na wazalishaji wa pembejeo za kilimo na mifugo, taasisi za fedha kwa ajili ya kutoa fursa ya upatikanaji wa mitaji ya masharti nafuu ya kuwekeza katika sekta ya kilimo, mifugo na mazingira.

Wadau wengine amewataja kuwa ni taasisi za utafiti katika sekta ya kilimo na mifugo, wasindikaji na wafanyabiashara katika sekta ya kilimo na mifugo, mashirika ya serikali na yasiyo ya kiserikali yanayojihusisha na shughuli za kilimo, mifugo na mazingira, taasisi za umma na binafsi zinazotoa huduma ambatano kwa wakulima na wafugaji ikiwemo taasisi za Bima, hifadhi ya jamii na nishati safi ya kupikia.

Dhamira kubwa hapa ni kutekeleza maono ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuhifadhi mazingira hapa nchini, kuondoa umasikini kwa watanzania, kukuza uchumi wao na kuongeza ukusanyaji wa mapato kwa maendeleo ya Taifa na watu wake.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.