• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SEKTA YA AFYA YAPUNGUZA VIFO MKOANI MOROGORO

Posted on: May 24th, 2024

Sekta ya Afya Mkoani Morogoro imeweka mikakati ya kuwawezesha Wauguzi kutafuta mbinu za kupunguza vifo vya Mama na Mtoto vinavyotokana na uzazi kwa kufuata kanuni na taratibu za kuwahudumia wananchi.

Hayo yamebainishwa Mei 24, 2024 na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa katika maadhimisho ya siku ya wauguzi Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Kituo cha Afya cha Sabasaba kilichopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mkoani humo.

Dkt. Mussa amesema vifo vya Mama na Mtoto vimepungua kutoka 115  hadi  85 kwa mwaka 2022/2023 kwa kila watu laki moja na kuwataka wauguzi kuendelea na jitihada hizo za kupunguza na ikiwezekana kukomesha kabisa vifo vinavyotokana na uzazi.

"...hadi sasa takwimu zinaonesha mmefanikiwa kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kutoka 115 hadi 85 kwa kila watu laki moja kwa mwaka 2022 hadi 2023..." amesema Dkt. Mussa.

Aidha, Dkt. Mussa amewataka wauguzi kujiendeleza kielimu kwa kutumia elimu za kimtandao (Online Education)  ili kuwa na wakati mzuri wa kuendelea na kazi sambamba Mkoa kutokuwa na uhaba wa wafanyakazi katika vituo vya afya.

Katika hatua nyingine, Katibu Tawala huyo ameishauri sekta ya Afya Mkoani humo kuanzisha miradi mbalimbali ikiwemo mashamba ya miti ya kudumu likiwemo zao la Karafuu na Kokoa na kuahidi kutoa bure eneo kwa ajili ya uwekezaji huo.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kusirye Ukio amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imetumia au kuwekeza Tsh. Bil. 30 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya sekta ya Afya.kwa miaka mitatu mfululizo

Ameongeza kuwa pia Serikali imetenga ama kuwekeza Tsh Bil.10 kwa ajili ya kununuzi wa madawa kwa kipindi cha miaka miwili huku akisisitiza watendaji wa Sekta ya Afya wa Hospitali na Vituo vya afya kusimamia vyema utoaji wa huduma kwa wateja (Customer care) kwa kutumia lugha yenye matumaini.

Nae, Katibu wa Chama cha Wauguzi Mkoa wa Morogoro Dkt. Awadhi Juma Utime amesema Mkoa wa Morogoro una jumla ya wauguzi 1737 katika vituo mbalimbali vya Afya huku akibainisha upungufu wa Wauguzi 4297 na kuiomba Serikali kuangalia namna ya kutatua changamoto hiyo ya upungufu wa Wauguzi.

Maadhimisho hayo ya wauguzi duniani yamefanyika Mkoani Morogoro yakiwa na kaulimbiu isemayo "Wauguzi sauti inayoongoza wekeza katika uuguzi, heshimu haki na Linda haki".

Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.