• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Sensa ya majaribio Morogoro yavuka lengo

Posted on: September 17th, 2021

Zoezi la sensa ya majaribio ya watu na Makazi katika Mkoa wa Morogoro limefanyika na kufanikiwa kwa zaidi ya asilimia 100 baada ya kaya zilizokusudiwa kuhesabiwa kuzidi matarajio ya wajumbe wa kamati ya sensa ya Mkoa huo.

Hayo yamebainishwa Septemba 16 mwaka huu na Mratibu wa Sensa wa Mkoa huo Charles Mtabo wakati akitoa taarifa ya zoezi hilo kwa Kamati ya Sensa ya majaribio ya Mkoa ilipotembelea eneo la zoezi Mtaa wa Mtawala katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa ajili ya kuangalia maendeleo ya zoezi hilo.


Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Bi. Mariam Mtunguja (wa pili kulia) akiwa na wajumbe wa kamati ya sensa ya majaribio Mkoa wa Morogoro katika Mtaa wa Mtawala Kata ya Mwembesongo.

Akifafanua zaidi, Mtabo amesema jumla ya kaya 332 za Mtaa huo zimehesabiwa kwenye zoezi hilo hivyo kuvuka lengo la kaya 300 zilizokuwa zimelengwa  kuhesabiwa katika Mtaa huo uliopo kata ya Mwembesongo.

Katika hatua nyingine, Mtabo amebainisha kazi mbalimbali zinazofanyika katika sensa hiyo ya majaribio kuwa ni pamoja na kutambua mipaka ya kuhesabu watu, kuendesha sensa ya watu na makazi kwa wakazi wote waliolala usiku wa kuamkia siku ya sensa na kuendesha zoezi la kupata Anuani za makazi.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Bi. Mariam Mtunguja ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya Sensa ya Mkoa amesema kufanikiwa kwa zoezi hilo kwa zaidi ya asilimia 100 ya kaya zilizohesabiwa zinatokana na hamasa iliyofanyika katika kutoa  Elimu kwa wananchi wa mtaa huo juu ya umuhimu wa zoezi la sensa ya majaribio.


Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Bi. Mariam Mtunguja (kushoto) akizungumza na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Morogoro.

Aidha, amewapongeza wananchi wa mtaa wa Mtawala na kuwataka kuwa mabalozi wakati wa sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika Agosti 27 kuamkia 28, 2022 ili kuisaidia Serikali ya Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupanga bajeti nzuri itakayokidhi huduma zote za kijamii kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

‘’Bila uhamasishaji zoezi hili halitofanikiwa, kwa hiyo sisi tunajipanga kufanya uhamasishaji wa nguvu kwa kushirikiana na viongozi wa Mkoa huu’’ amesema Mtunguja.

Kwa upande wake Mshauri wa Bodi ya Wajumbe wa Sensa Dkt. Nicolaus Shombe,  ameeleza kuwa sensa ya mwaka huu ni tofauti na nyingine zilizopita kutokana na zoezi hilo kuhusisha wajumbe wa zoezi hilo kutoka eneo husika.

‘’Kama labda unaenda sehemu ambayo ni jamii ya wafugaji watatumika watu wa jamii hiyo, kwa hiyo hata tukienda kwenye makundi ya watu maalum watatumika watu hao ili kuondoa dhana potofu walionayo baadhi ya watu katika zoezi hili’’ amesema Shombe.

Naye Msimamizi wa Sensa Kanda ya Pwani na Morogoro Dkt. Joyce Peter amebainisha umuhimu wa kutambua Anuani za makazi katika jaribio hilo kuwa ni kusaidia kutambua sehemu anapoishi mtu kwa urahisi ili kufikisha taarifa ama huduma mbalimbali zinazotolewa na Serikali.

Akizunguzia namna ambavyo zoezi hilo liaendelea kufanyika  Afisa Mtendaji wa Kata ya Mwembesongo  Amina Said ambaye pia ni Katibu wa Sensa ngazi ya kata hiyo, amesema zoezi hilo limefanyika kwa ufanisi na watahakikisha changamoto chache zilizojitokeza wanakabiliana nazo ili mwakani zoezi hilo lifanyike kwa ufanisi zaidi.

Sensa ya watu na Makazi hapa nchini inatarajiwa kufanyika mwakani agosti 27 kuamkia 28 ambapo mwaka huu serikali imeteua mikoa 13 hapa nchini kwa ajili ya kufanya sense ya majaribio ya watu na makazi ukiwemo Mkoa wa Morogoro katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kata ya Mwembesongo Mtaa wa Mtawala.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.