• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

SERIKALI IMEENDELEA KUBORESHA SEKTA YA MADINI - RC MALIMA.

Posted on: November 13th, 2024



Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kuboresha sekta ya madini hivyo, wachimbaji wadogo wametakiwa kuchangamkia fursa zilizopo kwenye sekta hiyo na kuzingatia tafiti za uchimbaji madini kulingana na  mabadiliko ya kisayansi yaliyopo kwenye sekta hiyo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima Novemba 13, 2024 wakati akifungua mkutano wa wadau wa madini Mkoa wa Morogoro uliofanyika katika ukumbi wa  hoteli ya Uluguru katika Manispaa hiyo ukiwa na lengo  la kuhamasisha shughuli za uchimbaji wa madini ndani ya Mkoa huo.

Kwa sababu hiyo amewataka wachimbaji wadogo kutumia fursa ya kipindi hiki cha Serikali ya awamu ya sita kuchangamkia fursa hiyo ya sekta ya madini kujiunga pamoja, kuchukua mikopo banki na kuendeleza shughuli zao za uchimbaji.

".. Bado nawahimiza msiache mbachao kwa msala upitao, fursa iliyopo kwa sasa hivi kwa maendeleo ya sekta yenu ni kubwa sana nakuombeni muitumie.." amesisitiza Mhe. Adam Malima.

Aidha Mhe. Malima amekemea tabia ya baadhi ya wachimbaji wa madini kuchimba  kwa kutozingatia taratibu na kanuni jambo ambalo hupelekea uharibifu wa vyanzo vya maji na kusababisha madhara kwa watumiaji wa maji kwa ujumla.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa Mhe. Adam Malima amewaahidi wachimbaji wa madini mkoani humo kuwapa ushirikiano wa kutosha hususan wakati wanapopata changamoto zikiwemo changamotoza za mikopo kwa lengo la kuwaendeleza na kuwainua kwa maslahi mapana ya Taifa.

Katika hatua nyingine Mhe. Malima amefurahishwa na ongezeko la wachimbaji wa madini wakike na kuwapongeza wachimbaji hao kwa kujitoa kufanya kazi hizo ambazo huwapatia kipato chao na kuongeza pato la Mkoa.

Kwa upande wake Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Morogoro Bi. Zabibu Napacho amesema katika Mkoa wa Morogoro kuna jumla ya leseni za uchimbaji wa madini 2413 ambapo leseni 205 zinafanya kazi na leseni 2208 hazifanyi kazi, aidha Mkoa una jumla ya leseni za tafiti za madini 61 ambapo 18 zinafanya kazi na 43 hazifanyi kazi.

Pia kiongozi huyo ameiomba Mamlaka zinazo shughulikia maji, Barabara na Umeme kuboresha miundombinu katika maeneo ya migodi ili kuweza kufanya kazi mbalimbali zikiwemo za usafiri na usafirishaji kwa urahisi.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Madini Mkoa wa Morogoro (MOREMA) Dr. Mzeru Omari ameeleza changamoto wanazokutana nazo wachimbaji wadogo kuwa ni pomoja na ukosefu wa soko kwa ajili ya kufanya biashara ya madini huku akiiomba Serikali kuwapatia vifaa vya kisasa vya upimaji na utambuzi wa madini chini ya ardhi ili kuondokana na uchimbaji wa madini wa kubahatisha.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.